All Sermons
Bible Passage Mathayo 13:24-30
This content is part of a series Mahubiri, in .

WAKATI NI KILA KITU

Date preached June 8, 2025

WAKATI NI KILA KITU
Mathayo 13:24-30

 

Nilianza kuwaza kuwa na shule ya Biblia miaka mingi sana lakini Sidhani kama nilijua kwamba mambo mazuri huhitaji muda

Nilipokuwa mdogo sikuwa na subira lakini sasa naelewa mambo mazuri yanahitaji muda

Mambo madogo madogo kama chakula huhitaji maandalizi na maandalizi yanahitaji muda

Siku hizi watu hawana muda wa kupika lakini wanakula

Hata watu wa kufanya nao kazi unahitaji muda kuwapata

Mambo mazuri huhitaji muda

Una pesa lakini huna hekima sio muda utabaki na hela bila watu

Kukua kunahusiana na mafunzo unayojifunza unapopanda juu

Kuna mambo unajifunza huku unapambana na kuna vitu unajifunza wakati unapitia majaribu

Inachukua muda kufanya vyema na kwa hakika inachukua muda kuwa vizuri.

Muhubiri 3:1-2

Kila jambo lina wakati

Kila jambo lina majira

Kila kusudi lina wakati; Unapokuwa na kusudi, unajua wakati wa hilo kusudi?

Ni lazima tuelewe kwamba hata watu wapo ambao ni kwa ajili ya wakati na kusudi

Wengine ni kwa ajili ya majira Fulani yamaisha yako

Fursa fulani ni za majira fulani

Kama vile majira na nyakati zibadilikavyo ndivyo tunatakiwa kujua kwamba majira na maisha hubadilika na yanapobadilika usifikirie kwamba Baraka zimeisha

Baraka hazijakoma ila ni majira yamebadilika

Nikipata muda nitazungumzia ulinganifu wa majira ya kuzaliwa na msjira kufa

Wakati wa kupanda na wakati wa kungíoa kilichokuwa kimepandwa
Je unaelewa utofauti wa maisha yako?

Je maisha yako yana majira na nyakati?
Utofauti wa kujua majira na nyakati za kupanda na kungíoa

Umewahi kumwomba Mungu ili akupe kujua wakati na majira sio ya mwaka bali majira na nyakati za maisha yako?

Au dhamira yako ni kutunza yaliyopandwa?

Dhamira yako ni kutunza uliyoyazoea na huwezi kuupa mkono wa kwa heri Wakati na majira uliyokuwa nayo

Unatunza yaliyopandwa hadi yakufie

Ni lazima uwe na roho ya kuachilia bila kugombana ili kukumbati majira ambayo Mungu anataka kuyaong’oa

1Kor. 13:11-12

Majira ya utoto

Kama bado unawaza kama ulivyokuwa unawaza wakati una miaka 10, habari mbaya ni kwamba una ulemavu rohoni na ulemavu huo unayazuia mawazo kuongezeka na yanabaki kwenye kipimo kile kile

Unajiuliza inawezekanaje? Ni kwasababu kama Unangíangíania majira na nyakati unayachelewesha majira mapya maishani mwako

Kuishi kwenye majira na nyakati zako ni jambo muhimu sana

Wakati ni kila kitu!

Sema, Mungu nifundishe nijue nyakati na majira yangu

Unaweza kuwa sahihi unachoongea lakini ukawa sio wakati sahihi wa kusema

Taarifa zingine zitasababisha nyumba ianguke

Mtoto ajisikie kunyanyaswa

Wakati ni kila kitu Waefeso 4:17

Ni lazima ufanye kila jambo kwa wakati na majira yake vinginevyo hutakuwa na matokeo unayoyatamani

Je unafahamu saa hizi ni majira gani kwenye maisha yako?

Kuna saa maishani mwako inayosoma majira na nyakati za maisha yako

Nina saa mkononi inayoniwezesha kujua ni saa ngapi lakini unajua ni saa ngapi maishani mwako

Katika utumishi wako?
Katika Ukristo wako?

Je ni wakati wa kungíoa?

Je ni wakati wa kupanda?

Umuhimu wa maswali haya ni kwamba unaweza tu kuzaa matunda ndani ya majira yako

Kanisa linaweza kuzaa kama lipo ndani ya nyakati na majira

Cha muhimu hapo ni kwamba hakuna matunda yanayopatikana nje ya majira na nyakati

Ni lazima ujue nyakati za kungíangíania na nyakati za kukunja

Bila kujali ni aina gani ya mti uko juu ya ardhi, kunakuwa na mizizi iliyoshikana ardhini

Hata magugu yana mizizi lakini mizizi ya magugu ni mikubwa kuliko mizizi ya ngano

Kabla sijaingia kiundani nataka ujiulize kwa nini unajifunza somo hili hata kama umesoma hii aya siku zote

-Je hii nafasi inamaana gani kwangu?

-Mungu anakukumbusha kwamba uko katika majira gani?

Waebrania 5:11-12

Wakati wa kukua

Ukiheshimu Wakati na majira yako utaheshimu saa yako ya mkononi

Usipoheshimu hutaheshimiwa, hutaheshimika,hutafanikiwa kiuchumi, hutakuwa na nguvu

Ni wale tu masikini ndio wanaokuwa masikini wasipoanza kuheshimu majira na nyakati za maisha yao

Hao ndio ambao wakati wanaokuwa nao ni ule wakifumbua macho kutoka usingizini

Sasa turudie kusoma Mathayo 13:24-30

Walipolala
Adui ndipo alipopanda magugu- wakati Fulani nimekuwa nikihubiri kinyume na waliolala uzingizi hadi niligundua kwamba binadamu wote huwa tunalala usingizi

Ila ni jambo la hatari kulala usingizi nyakati ambazo sio majira ya kulala usingizi

Hata hivyo wengine wanalala

Hapa tunaona kwamba watumwa hawagundua asubuhi kulipokucha kwamba kuna mabadiliko shambani

Kuna nyakati na majira hutarajiwi kulala
ìOmbeni msije mkaingia majaribuniî Hata hivyo alikuta wamelala

Hata walipoamka asubuhi hawakugundua kama Adui alikuja pale achilia mbali kujua kama kuna mbegu za magugu zimepandwa

Adui alipanda wakati wamelala, na alipanda katika namna ambayo hata wakiamka wasigundue mabadiliko yoyote

1. KUPANDWA KWA HAKUONDOI KUPANDWA KWA MAJASUSI YA SHETANI
Matendo 20:28-32

Jambo jema huvutia baya

Mungu akiruhusu ngano kupandwa haimaanishi kwamba magugu yamezuiliwa

Kwa hiyo tunatakiwa kuzaa matunda mbele ya magugu

Kwako wewe unayesubiri magugu yaishe ndipo uzae matunda huchimbi hii aya kwa sababu aya hii inaonyesha kwamba hakutakuwa na siku maishani mwako ambapo hutakuwa na magugu

Ngano zilipandwa kwa malengo kwa maneno mengine ni kwamba ngano isingeota pale kama isingepandwa pale kwa sababu pale sio asili yake

Kuota ngano pale sio tokeo la hali ya asili ya hewa,udongo, mvua, jua. Kuna mtu aliamua kupanda mbegu ya ngano

Mvua haikuwa na mbegu ya ngano

Hewa haikuwa na mbegu ya ngano

Udongo haukuwa na mbegu ya ngano

Jua halikuwa na mbegu ya ngano

Tena,

Usifikiri magugu yalijiotea; Biblia inasema Adui alikuja kupanda magugu. Kwa hiyo hata magugu pale shambani hapakuwa asili yao

Kuna jitihada na timing ilifanyika

Mafanikio yanahitaji muda lakini yana mapambano

Ushindi unahitaji muda

Kupanda cheo kunahitaji muda

Uinjilisti, Ukristo, uongozi, ni jasho

Waliopanda ngano usidhani hawakutokwa jasho

Na aliyepanda magugu usidhani hakutokwa jasho

“Agriculture” ni intentional= Dhamira

Dhamira ya kupanda mbegu ni kupata ngano na dhamira kupata ngano ni kupata mkate

Mbegu—-Ngano—Mkate

Huwezi kupanda mbegu leo na kupata kula mkate jioni kwa sababu kila kitu kinahitaji muda. Kuna nyakati za kusubiri na majira ya kuvuna

Kuna nyakati za Subira ili kupata majira ya kuvuna

Kwa hiyo, kama unataka kuwa na matunda ni lazima ukue kwenda chini kwanza kisha juu

Wengi mnaacha kupanda kwa sababa kila ukiangalia nyumba huoni mbegu inayoota

Mbegu huota kuanzia chini na hukua chini kwanza. Mizizi haikui kupanda juu na majani hayatangulii mizizi

Ukisubiri Mbegu itabadilika kuwa ngano na kuwa mkate

Kuna kazi katikati ya kila hatua. Kupanda ngano ni kazi na kuvuna ni kazi

Huwezi kula vizuri kuliko unavyovuja jasho

Kuhusiana na Ahadi za Mungu (Mathayo 28:20) unapaswa kutambua kwamba unatarajiwa kutoa jasho, unatarajiwa kufanya kazi

Unapaswa kusaga ngano kwa sababu ngano sio mkate hadi usage

Mwambie jirani “ninatoka kwenye hatua ya mbegu ili niwe ngano na kisha niwe mkate”

Inawezakana sionekani kama mkate lakini niko kwenye hatua

Naelekea mahali fulani kwenye majira ya maisha yangu

Usinidharau kwa sababu sijawa mkate, inawezekana sipo kwenye hatua ya kuwa ngano,inawezekana niko kwenye hatua ya mbegu lakini jambo moja la ukweli ni kwamba natoka hatua moja kwenda nyingine kwenye hatima yangu

Ni lazima ukubali kuwa tofauti, Ni lazima ukubali kusemwa

Tatizo kubwa tulilonalo leo ni wasiwasi

Tunaogopa kutengwa kuliko tunavyoogopa kutozaa matunda

Unatumia muda mwingi kumwomba Mungu juu yale wanayokusema na Mungu anasema usipojikana mwenyewe hufai-Adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake. Twende pointi namba mbili;

II. KILA PALIPO NA UWEZEKANO ZA MAVUNO ADUI ATAFUATILIA

Kupandwa ngano kulimfanya adui kuja kupanda magugu. Hakupanda magugu ili ngano zipandwe

Shetani alijua Mungu amekubariki, Kuzimu inajua Mungu anataka kukutumia, Kuzimu inajua Mungu ana kusudi na wewe ndio maana amekuwekea magugu maishani mwako

Mbegu za magugu zilipandwa kwa namna ambayo ni kama wapelelezi nyuma ya ngano na katikati ya ngano

Kila lililoharibika maishani mwako ilikuwa njia ya adui ili kukunasa

Sio kwa sababu ulikuwa na matunda bali kwa sababu ulikokuwa unaoenda ulikuwa unaelekea kuzaa matunda. Kwa hiyo alikuwahi

Alianza kuweka mifumo ardhini hata kabla mbegu ya ngano haijaota

Kabla huduma yako haijakua alihakikisha ameweka mifumo mahali ilipo mbegu ya huduma yako

Kabla hujawa mwaminifu 2Tim. 2:2
Adui aliweka miundombinu ili uwe na cha kupambana nacho

Kwa nini mambo ni magumu? Kwa nini napiga hatua mbili lakini narudi nyuma hatua kumi, Kwa nini kazi yangu ni ngumu sana wakati wengine huduma zao zinaenda kirahisi?

Ni kwa sababu Adui amepanda magugu katikati ya ngano

“walipolala” Adui akaja kupanda magugu

Kila palipo na ngano panakuwa na magugu

Kila palipo na mbegu za ngano adui anapanda mbegu za magugu

Na mbegu zote zilipandwa kwa matarajio

Hupambani na mapepo tu bali unapambana na mfumo wa mapepo uliowekwa na adui maishani mwako na sababu pekee ya kuwekwa mifumo hiyo maishani mwako ni kwa sababu wewe ni mbegu ya ngano

Wewe ni mbegu njema!

Shamba ni ulimwengu lakini mbegu zote sio za ulimwenguni. Mbegu unazopambana nazo sio za ulimwengu huu. Mifumo unayopambana nayo sio ya ulimwengu huu!

Waefeso 6:10-17

Shetani alipenya wakati wapandaji walipolala

Adui atasubiri mpaka asiwepo aliye macho kwenye familia yako, kwenye huduma, kanisani

Atasubiri kila mtu aondoke nyumani

Atasubiri mpaka uwe mpweke

Atasubiri mpaka wanaotarajiwa kuwa macho kwa ajili yako walale kwa sababu anatambua umuhimu wa wakati
“timing”

Kama alipannda wakati wamelala basi alipanda usiku, wakati wa giza

Sio tu mbegu alizopanda hazikuonekana, bali hata yeye hakuonekana anavyopanda

Wapandaji walipanda wakati kila mtu pamoja na adui wakiwa wanaona lakini adui alipanda wakati ambao wapandaji hawaoni na yeye mwenyewe hakuonekana. Alipanda gizani.

Na inawezekana wale wapandaji waliopanda mchana miongoni mwao adui alimtumia kupanda usiku-nawaza tu. Kwa sababu adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake

Giza la usiku lilimficha

Siwezi kuona aliyepanda magugu maishani mwangu lakini nayaona magugu

Siwezi kuona mbegu za adui lakini adui anaona mbegu zangu

Hila ya adui imeficha mbegu za adui chini ya ardhi

Wapandaji walipoamka asubuhi hawakuona dosari yoyote

Umewahi kujikuta jambo limeharibika nyumbani mwako, kanisani, maishani mwako lakini haijulikani lilianza lini kuharibika

Walipoamka asubuhi bila shaka walienda kumwagilia bila kujua kwamba wanamwagilia na mbegu za magugu

Sio tu adui alipanga mabaya kwa ajili ya ngano lakini pia alipanga kuzitumia nguvu na gharama za wapandaji na mwenye shamba kuotesha na magugu

Walipomwagilia hawakuona dosari yoyote hadi zilipoota.

Huo ndio wakati mfumo wa mizizi ulikuwa unajengwa. Kadri walivyomwagilia ngano ndivyo walivyomwagilia magugu kiasi ambacho mtandao ukawa mfumo kwenye udongo

Kabla mwaka haujaanza, mfumo utakaokusumbua umewekwa

Kabla ya Harusi na ndoa yako mfumo uliwekwa tayari

Kabla ya degree yako mfumo uliwekwa tayari

Kabla ya kuanza uinjilisti ulipomaliza mafunzo mfumo uliwekwa

Kwa hiyo Yesu anaposema nipo pamoja nanyi hata ukamilifu wa dahari katika Mathayo 28:20 na Marko 15:17-20 anamaanisha kwamba unapoinjilisha anatangulia kupambana na mfumo.

Hata ukipuuza haya shetani hatapuuza haya na atakuwekea mfumo

Kila siku mizizi ya ngano na mizizi ya magugu huingilina na kushikana ardhini

Kwa hiyo, Bwana Yesu anaposema “ufalme wa mbinguni umefanana na …” anasema ufalme wa mbinguni umefanana na vita iliyo chini kwa chini kabla haijatokea

Unajaribu kupambana juu ya ardhi (unapigana na damu na nyama), lakini vita unayoiona imewekewa mifumo na miundo mbinu chini ya ardhi (uliwengu wa roho)

Soma tena Waefeso 6:10-12

Mwambie jirani yako “vita unayoiona hapa ina mizizi rohoni”

Twende na mimi kwenye pointi namba tatu;

III. UHARIBIFU NA MAANGAMIZI NI VITU VIWILI TOFAUTI

Adui asingeweza kuua ngano ili isizae ngano na badala yake aliharibu mazingira ambayo kwa ngano ingemea

E Mungu wangu!

Adui alishindwa kukuzuia kuzaliwa lakini aliandaa
Mazingira magumu ya maisha yako

Mwambie jirani, “Adui hawezi kukuua ila atakutesa”

Hawezi kuua hatima yangu

Hawezi kuua kesho yangu

Hawezi kuua ambacho Mungu ameweka ndani yangu

Hawezi kulaani ambacho Mungu amekibariki! Ila jambo moja la uhakika ni kwamba ataharibu mazingira ya hatima yako,

Mazingira ya kesho yako

Mazigira ya maisha yako

Kama mizizi yangu ilibarikiwa na matunda yangu yatabarikiwa

Mchawi hawezi kukulaani

Mapepo hayawezi kukulaani

Kuzimu haiwezi kukulaani

Majaribu unayopitia hayawezi kukulaani

Watakulaani lakini hawafanikiwa kukulaani

Masengenyo yao hayawezi kukulaani

Waambie nimebarikiwa kwenye mizizi yangu, inawezekana huoni aliyonitendea Bwana lakini nimebarikiwa kwenye mizizi

Tangu tumboni mwa mama yangu nimebarikiwa

Uharibifu na maangamizi sio kitu kimoja. Inawezekana maangamizi ni matokeo ya uharibifu lakini sio jambo moja

Adui hawezi kuangamiza baraka zako bali ataharibu mazingira ya baraka zako

Umekuwa ukiomba na kumuuliza Mungu kwanini mambo yako yanarudi nyuma kwa namna yanavyorudi nyuma

Ni kwa sababu kuzimu ilijua umebarikiwa na jambo moja ambalo Adui anaweza kufanya ni kuharibu mazingira kwa kuweka mifumo ya miziz yake kwenye mizizi yako kabla hujashtuka, wakati umelala

Kabla hujaanza kuzaa matunda

Kabla ya kuwepo mwito maishani mwako

Kabla hujapandishwa cheo

Kabla hujaokoka, aliweka mfumo

Na kwakuwa shetani anaamini katika mbegu (Mawazo) kuliko watakatifu wanavyoamini katika mbegu

Watakatifu wangeamini katika mbegu matoleo yasingekuwa shida

Kile ambacho kinasisitizwa makanisani tayari kwenye ufalme kinajulikana kwamba huwezi kuvuna bila kupanda

Wagalatia 6:7-8
2Wakor. 9:6-10

Ukipanda haba utavuna haba

Na ya kwamba mti utautambua kwa matunda yake kwamba ni ngano au ni magugu

Usipoweka chochote hutatoa chochote

Wana wa ulimwengu wanaelewa haya yote na ni vigumu wana wa nuru kuyafahamu kwa sababu wana wa nuru hupanda mbegu mchana wakati adui naye anajifanya wa nuru na hivyo anaona lakini anachopanda adui gizani watakatifu wanakuwa wamelala 2Wakor. 11:7-11

Biblia inasema daima kutakuwa na majira ya mbegu na mavuno

Kila kitu kinatokana na mbegu

Na kama Adui angetaka kuingia kwenye eneo lako angepanda mbegu ya magugu na sio magugu

Shetani anajua unahangaika kufanikiwa bila mbegu ya mafanikio

Usisahau vita viko ardhini

Wapanndaji hawakujua mambo mawili kuhusu magugu
a) Magugu yametoka wapi
b)nia ya adui kupanda magugu kama ambavyo wengi manaosoma aya hii hamjui nia ya adui ilikuwa nini

“Wakamwambia Bwana wao magugu haya yametoka wapi?”

Unajiuliza kwanini najisikia hivi?

Kwa nini nina kichwa kigumu kuelewa vitu?

Kwa nini nimekuwa mzito kanisani?

Kwa nini nimekuwa mwepesi kuangalia mpira

Kwa nini napenda uimbaji kuliko neno la Mungu?

Ni kwa sababu kuna mfumo umetandazwa katika ulimwengu wa roho mahali ambako kuna mizizi yako inayokusaidia kuchipua duniani

Sasa tunajua kuna mtandao wa kimfumo,

Tunajua ni adui aliyepanda mbegu za magugu

Swali ni kwamba;

IV. KWANINI ADUI ALIPANDA MAGUGU WAKATI ANAJUA MAGUGU HAYAUWI NGANO?

Hili ni swali muhimu sana maana usipojua kwa nini shetani amekuwekea hiyo mifumo maishani mwako huwezi kushinda!

Mara ya kwanza nilidhani labda magugu yangeua ngano kwa kuisonga lakini ukweli ni kwamba ngano na magugu vilimea na kukua pamoja hadi ngano kufikia hatua ya mavuno

Kwa sababu kama ilikuwa ngano ilipoenda ardhini itamea ngano

Kama ulikuwa dhahabu unapoingia kwenye tanuru, utatoka ukiwa dhahabu

Na kama wakati inaingia ardhini ilikuwa magugu itamea magugu

Na kama magugu hayakuua ngano, na adui aiwa anajua, kwa nini alipanda magugu?

“Ufalme wa mbinguni umefanana na…”

Kama hawezi kulaani alichokibariki Mungu, kwa nini alipanda magugu tena usiku?

Kama hakuweza kubadili ngano kuwa magugu kwa nini alipanda mbegu za magugu

Kwa nini alijisumbua usiku kwenda kupanda mbegu za magugu pembeni ya kila mbegu ya ngano?

Mfumo haukutesi kwa sababu ya kuwepo magugu na ngano katika huduma yako, maishani mwako, kwenye familia yako, kwenye ndoa yako bali jaribu liko katikati ya ngano na magugu

Jaribu lako liko kwenye maamuzi utakayochukua dhidi ya magugu

Na ndio sababu ya adui kupanda magugu alipanda magugu ili kutega maamuzi ya mwenye shamba. Utanaswa kwenye maamuzi yako

Mtego uko kwenye swali “kwa nini adui alipanda magugu pembeni mwa mbegu ya ngano”

Wapandaji walipouliza kwa nini magugu yapo? Bwana wao alisema “adui amepanda magugu”

Wapandaji hawakujua magugu yalikotoka

Walichojua ni kupanda tu

Bwana wao alijua

Ni kama wapandaji hawakujua adui yao ni nani na anaweza kufanya nini

Wakamwambia “tukayang’oe”

Akawaambia “yaacheni” kwa sababu hata uking’oa magugu, miziz yake imeingiliana na mizizi ya ngano na hivyo uamuzi wa kung’oa magugu ungeua ngano

Adui alijua uamuzi utakaochukuliwa ni kung’oa magugu na waking’oa magugu watang’oa na matumaini yao

Sasa ambacho shetani anataka ufanye

Anataka ujiue mwenyewe!

Shetani anataka ujichukulie maamuzi mwenyewe ukidhani unapambana na maadui kumbe unapambana na mfumo aliokuwekea na ule mfumo umeenda chini na maamuzi ya kupambana nao utakuwa unaua ndoto zako mwenyewe

Utakuwa unaua familia yako mwenyewe

Utakuwa unaua huduma yako mwenyewe

Utakuwa unajinyonga mwenyewe

Mungu ameniambia nikwambie kwamba “nyamaza kimya”

Kukaa kimya kutageuza mtego lakini kupambana na mtego kutakuua

Sijui kama linakusaidia lakini hata kama unaona umevumilia umechoka, nyamaza kimya

Umechnganyikiwa jinsi mambo yanavyovurugika, nyamaza kimya

Umeibiwa wanasubiri upambane na mwizi, nyamaza kimya

Wamekudhulumu wanataka upambane nao, nyamaza

Umechoka na tabia za mwenzio, ukipambana naye utaua familia, utaua ndoto zako, utajinyonga

Shetani ameweka mpangilio wa kimfumo ndio maana tangu umeanza kupambana unapoteza nguvu na afya yako lakini hakuna linalobadilika,

Ukipambana utapata vidonda vya tumbo

Ukipambana utapata presha

Ukipambana wanajua utapambana kisha waripue mfumo waliokuzingira nao

Kunyamaza kwa Waisraeli ndiko kulikomzamisha Farao

Nguvu ya kutopambana na magugu ipo kwenye nayakati na majira

Ule haukuwa wakati wa kupambana na magugu

Wakati na majira ulipofika magugu yalichomwa moto

Inahitaji imani kunyamza

Adui anajua hawezi kukulaani ndio maana anataka kukutumia mwenyewe ili ujiue mwenyewe

Mungu anasema nyamaza kimya

Vita ni vya Bwana!

Shetani hawezi kukuzuia usifanye uinjilisti lakini amekuwekea mtego wa kujitilia mashaka mwenyewe

Uing’oa magugu unang’oa na ngano

Unapojaribu kulitengeneza unaharibu zaidi

Usinaswe na mtego wa kukosa uvumilivu

Imani yako inaonekana katika ukimya na kusema sema ni ishara ukosefu wa imani

Hivi sio vita vyako,

Uamuzi wa kung’oa magugu haukutakiwa kutoka kwa wapandaji bali kwa aliyewatuma

Adui amekuwekea moyo wa haraka na pupa lakini leo nataka nikwambie alichiniagiza mungu nikwambie;

Mbegu unayoweza kupanda wkati unapanda ngano ni wakati. Ukipoteza fedha unaweza kupata zingine tena lakini ukiharibu wakati huwezi kuupata tena. Ukipanda wakati, wakati utakupatia majira ya kupata fedha

Uking’oa magugu utapoteza mavuno ya ngano

Bwana anajua jinsi ya kushughulikia magugu, hayashughulikiwi sasa! ni swala majira na nyakati

Kwa sababu umechanganyikiwa na umechoshwa na hujui hata unapambana na nini
Huelewi kwa nini unapambana

Huelewi hata vita yenyewe ilivyoanzaje

Adui anataka ufanye maamuzi na hujui ni maamuzi yapi hayatakudhuru

Mungu anasema usifanye uamuzi wowote kwenye hali hiyo. Tulia nyamaza kimya.

Kukaa mimya hujakosea, ni kusema huu sio wakati wa kufanya maamuzijuu ya magugu

V. MAVUNO HAYAHARAKISHWI NA DHARULA YA MPANDAJI

Mavuno yatakuja.
Haifai kung’oa magugu kabla ya mavuno ya ngano

Ukiyang’oa kabla ya mavuno, unaua mavuno

Majira uliyonayo sio ya kung’oa lakini kuna majira ya kung’oa yanakuja. Kwa sasa nyamaza

Majira yakifika utang’oa bila kusababisha hasara

Mungu ameniambia ni kwambie kwamba unaelekea kwenye nyakati za mavuno

Na kinachofanya uchanganyikiwe ni magugu kuonekana hayavumiliki wakati umeyavumilia miaka yote hii

Hayavumiliki kwa sababu kadri mavuno yanapokaribia ndivyo magugu yanavyorefuka na kuonekana kuliko ngano. Ndivyo ukweli unavyofichwa chini ya majungu na uongo na uzushi

Unakaribia kuvuna ngano

Kanuni ya Mungu inasema “unapanda kwa machozi unavuna kwa furaha”

Hakuna njia nyingine ya kuvuna isipokuwa kwa furaha ndio maana adui anataka usivune ili ukose furaha

Anataka kukupokonya furaha yako

Nyakati ambazo unataka kujitetea, nyamaza kimya

Jambo gumu kulifanya ni kunyamza wakati adui anapokufanya ulipize

Kuna mashambulizi mengine yanakujia ukiwa kwenye njia sahihi na njia bora ya kushughulika nayo ni kutokushughulishwa nayo

Kwa sababu:
1. Sio majira ya kung’oa
2. Ni mtego

Nyamaza ukimtwika Yesu mafadhaiko yako yote

Omba na kufunga ili Mungu akupe ujasiri wa kungoja

Haraka unayoisikia ndani yako inakuingiza kwenye mtego

Umepitia mengi yamekukondesha

Adui hakupanda magugu ili avune magugu. Kwa hiyo hana faida na magugu ila anataka usivune ngano

Ataitumia pupa uliyonayo kukukosesha mavuno

Unatakiwa uelewe kwamba Adui hawezi kukulaani ila anaweza kukutumia ili ujilaani mwenyewe

Hasira zako, ulimi wako vinaweza kulaani ambavyo ni baraka zako

Adui anajua silaha kubwa aliyonayo dhidi ya watu wa Mungu ni watu wa Mungu

Sila ya adui juu ya maisha yako ni maisha yako

Silaha ya adui juu ya familia yako ni familia yako

Silaha adui juu yako ni wewe mwenyewe

Kama huwezi kupata furaha sasa hutapata furaha tena

Baadhi yenu Mungu amewavusha na korona

Kumbuka Wakati ni kila kitu

Adui asikupumbaze kufanya maamuzi mabaya

Jenga imani kwa Mungu.

Atakamilisha alilolianzisha ndani yetu

Hujasahauliwa, hujaachwa

Najua inatishakuzungukwa na magugu

Lakini nikutie moyo, hakuna silaha itakayofanikiwa dhidi yako

Amini tu ngano itakuwa mkate

Mavuno hayachelewa kama mtego utakavyokuchelewesha

Usiziamini hisia zako

Mwonyeshe Ibilisi ajue kwamba ulienda aridhini ukiwa ngano na utatoka kama ngano

Mbegu-ngano-mkate

Sitaacha mpaka nione tumaini la wito wangu

Nakuombea siku zote kwamba;

Roho ya uvumilivu iwe juu yako

Roho ya manung’uniko na malalamiko ikome

Ukimya na ujasiri vikawe nguvu yako

Nguvu haiko katika kelele

Kwa Jina la Yesu Kristo!

Sijui hatima yako ni nini

Sijui Mungu amekuandalia nini

Lakini ninachojua ni kwamba kama Mungu asingekuwa na makusudi na wewe wangekumeza ungali hai kwa jinsi walivyo na chuki hata kama unawasaidia

Acha manunguniko

Ishi kama vile hakuna vita

Pumua, hema!

Amani iwe juu yako

Subira iwe juu yako

Unakaribia kuvuna kuliko ilivyowahi kuwa maishani mwako

Wakati wa mavuno ndipo utakapotenganisha ngano na magugu

Adui anapotaka kukutumia kujiua wewe tumia subira kama silaha ya kuua mbegu za adui kwenye familia yako, kwenye huduma yako, kwenye biashara yako, Kwenye maisha yako

Lakini wewe ni nani kwenye huu mfano?

Wewe ni nani?
1. Watumwa waliopanda
2. Mbegu njema
3. Adui
4. Magugu

Barikiwa!

 

In series Mahubiri