“Na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine.” – 2 Tim. 2:2
“Lihubiri neno, uwe Tayari wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote…Bali wewe uwe na kiasi katika mambo yote, vumiia mabaya, fanya kazi ya muhubiri wa injili, timiliza huduma yako” 2Tim. 4:2,5
Tuna namna mbalimbali za kufikia shauku ya kujifunza Biblia. Tuna programu ya miaka miwili hadi mitatu kwa wanaojifunza Theolojia na Biblia,
Mwaka mmoja kwa wote bila kujali dini zao wanaojifunza Biblia tu
Masomo ya kujaza ukiwa nyumbani (utaletewa au kutumiwa ulipo). Program zote hizi zitakuhakikishia unafanikiwa katika lengo lako la kutaka kujifunza. wasiliana nasi leo. Kozi ya Theolojia na Biblia ni kwa malipo lakini kozi zingine zote ni bila malipo.
Falsafa ya masomo katika shule ya Theolojia na Biblia: –Hii ni shule iliyoundwa ili kumpatia mwanafunzi wa Neno la Mungu elimu ya Biblia kwa kina na mapana. Masomo yaliyopo ni yale yatekwayo kama maji kutoka kwenye Biblia. Masomo haya ni kwa ajili ya mtumishi wa Mungu yeyote anayependa Neno la Mungu. na kumtumikia
Tunakukaribisha kwa moyo mkunjufu katika shule yetu, ni mahali pa amani, upendo, na uwepo wa Mungu.
Kanisa la Kristo Yesu Ulimwenguni ni familia ya waumini wanaomtumikia Mungu kwa Roho na kweli, Kwa kujengwa na Neno lake, na wakipendana bila ubaguzi.
Katika dunia yenye mgawanyiko na maumivu, upendo wa Kristo ndio daraja letu. Ni nguvu inayoshinda chuki, ni mwanga unaofukuza giza, ni mnyororo wa neema unaotufanya kuwa familia moja – bila kujali rangi, kabila, hali, au historia.