Kanisa la Kristo Yesu Ulimwenguni

“Na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa  kuwafundisha na wengine.” – 2 Tim. 2:2

“Lihubiri neno, uwe Tayari wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote…Bali wewe uwe na kiasi katika mambo yote, vumiia mabaya, fanya kazi ya muhubiri wa injili, timiliza huduma yako” 2Tim. 4:2,5

Hadithi ya kweli ya kesho yako

Kila mmoja wetu ana safari yake ya kipekee ya imani. Tunaamini kuwa ushuhuda wako unaweza kuwa chombo cha kubadilisha maisha ya mtu mwingine.
Ungana nasi

Idara za Kanisa

Katika Kanisa la Kristo Yesu tuna vikundi na idara mbalimbali ili katimiliza huduma ya injili; Idara hizo ni; 1. Idara ya maombi 2. Idara ya Uinjiliti na Umisheni 3. Idara ya Elimu ya Maandiko na Elimu dunia 4.Idara maalumu ya uchaguzi na maadili Idara hizi zinaundwa katika ngazi ya kimataifa , Kitaifa na kushuka kwenye ngazi za mikoa, wilaya na hadi kusanyiko la mahali pamoja
Ungana nasi

Kanisa letu na jamii

Nguzo na msingi wa Kanisa la Kristo Yesu ni Mathayo 28:18-20; Marko 16:15-20; Matendo 1:8 na 2Tim. 2:2 Tunagusa maisha ya jamii kwa huduma za kijamii kama; Chekechea, mafunzo ya uajasiriamali, Kilimo cha mbogamboga, mafunzo ya ufundi kwa vijana, na wajane.
Ungana nasi

Uinjilisti

Pamoja na maombezi, Tunatoa masomo ya Biblia kwa vipeperushi, majarida, darasani , masafa, na nyumba kwa nyumba. Hii ni pamoja na mahubri na ushauri nyumba kwa nyumba mtu kwa mtu

Huduma kwa Jamii

Ushauri nasaha, mafunzo ya ufundi, na ujasiriamali. Hii ni pamoja na kanisa kujitoa kwa ajili ya kusaida mahitaji ya papo kwa papo na ya muda mrefu kama chekechea na Kilimo

shiriki

baraka za
Mungu. gharamia kazi ya Mungu

Tembelea ibada zetu

Tunakukaribisha kuabudu na sisi. Ukiwa Sumbawanga tembelea Kanisa la Kristo Yesu Sumbawanga mjini; ukiwa Songwe tembelea Kanisa la Kristo Yesu Mpui na Isunda; Ukiwa Nkasi tembelea Majengo na Lunyala; Ukiwa Dodoma tembelea Kanisa la Kristo Yesu Iyegu; Ukiwa kikunde tembelea kanisa la Kristo Yesu Kikunde; Ukiwa mbeya tembelea Uyole Ibada zetu ni Jumapili kuanzia saa 3:30 asubuhi-saa 6.00 Mchana na Jioni saa 11.00-12.00 jioni. Siku za katikati ni Jumatano saa 11:00-12.00 darasa la Biblia (maswali na majibu)

Hapa ni kama nyumbani ukitutembelea

Mafundisho na mahubiri yetu sio mwisho wa kila kitu. msilizaji anaruhusiwa kuhoji ama kuuliza maswali yatokanayo na alichokisia ama alichokisikia kwenye kipindi au ibada. Majibu yatatokana na Neno la Mungu tu na kama jibu kwa siku hiyo halitatosheleza mwalimu atakuahidi kwenye kufanya utafiti na kurudi kukujibu ama kukutembelea nyumani. Sisi ni familia pamoja ni familia ya Mungu.

Masomo mbalimbali

“Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.” – Warumi 10:17

Karibu mno

Salimianeni kwa busu takatifu, makanisa yote ya Kristo yawasalimu

Mungu no roho nao wamwabuduo imewapaswa wabudu katika Roho na kweli

Tunaabudu katia Roho kwa kunyenyekea na kujimimina mbele za Mungu katika uimbaji, Maombi, Mahubiri, Meza ya Bwana na Kutoa mali zetu lakini wakati huohuo tunafanya yote hayo kwa kuhakiki katika Neno kama tunachofanya ndicho tulichoamuriwa na Mungu.
"Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike kwa kuwa walilipokea lile Neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kama mambo haya ndivyo yalivyo" Matendo 17:11

"Nimkaribie BWANA na kitu gani, na kuinama mbele za Mungu aliye juu? Je, nimkaribie na sadaka za kuteketezwa, na ndama za umri wa mwaka mmoja...Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na BWANA anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako.

Imani Inayofanya upya Maisha

Katika Kanisa la Kristo Yesu Ulimwenguni, tunaamini kuwa imani si hisia tu bali daraja linalokukutanisha na moyo wa Mungu

Jiunge na Shule yetu ya Biblia

Tuna namna mbalimbali za kufikia shauku ya kujifunza Biblia. Tuna programu ya miaka miwili hadi mitatu kwa wanaojifunza Theolojia na Biblia,
Mwaka mmoja kwa wote bila kujali dini zao wanaojifunza Biblia tu
Masomo ya kujaza ukiwa nyumbani (utaletewa au kutumiwa ulipo). Program zote hizi zitakuhakikishia unafanikiwa katika lengo lako la kutaka kujifunza. wasiliana nasi leo. Kozi ya Theolojia na Biblia ni kwa malipo lakini kozi zingine zote ni bila malipo.

Falsafa ya masomo katika shule ya Theolojia na Biblia: –Hii ni shule iliyoundwa ili kumpatia  mwanafunzi wa Neno la Mungu elimu ya Biblia kwa kina na mapana. Masomo yaliyopo ni yale yatekwayo kama maji kutoka kwenye Biblia. Masomo haya ni kwa ajili ya mtumishi wa Mungu yeyote anayependa Neno la Mungu. na kumtumikia

Tunakukaribisha kwa moyo mkunjufu katika shule yetu, ni mahali pa amani, upendo, na uwepo wa Mungu.

Kanisa la Kristo Yesu Ulimwenguni ni familia ya waumini wanaomtumikia Mungu kwa Roho na kweli, Kwa kujengwa na Neno lake, na wakipendana bila ubaguzi.

Upendo wa Kristo Unatuunganisha

Katika dunia yenye mgawanyiko na maumivu, upendo wa Kristo ndio daraja letu. Ni nguvu inayoshinda chuki, ni mwanga unaofukuza giza, ni mnyororo wa neema unaotufanya kuwa familia moja – bila kujali rangi, kabila, hali, au historia.

Ibada ya Roho na Kweli

Tunamwabudu Mungu kwa uhuru na kwa moyo wa kweli, tukiongozwa na Roho Mtakatifu. kuliko kuongozwa na mazoea au magizo ya wanadamu

Familia ya Kiimani

Hapa unakuwa sehemu ya jamii inayokupenda, kukuombea, na kukuinua.

Mahali pa Kukua Kiimani

Hatuishii katika kukusikiliza tu – tunakusaidia kuchukua hatua, kutumia ili upate wokovu na kuona kipawa chako, ili kutimiza kusudi la Munu maishani mwako.

Ufundishaji wa kina na mapana wa neno la Mungu

Kila ibada ni nafasi ya kuunganishwa na Mungu. Lengo letu kuu ni kuhakikisha kuwa Neno la Mungu linafundishwa kama inavyotakiwa kwa kuzingatia mazingira ya kihistoria, Jiografia, jamii wakati wa aya kuandikwa na kuona mazingira ya karibu ya aya ambayo nimaisha ya msikiaji wa leo

Jumapili – Ibada : Saa 3:30 Asubuhi – 6:00 Mchana