All Sermons
Bible Passage Luka 5:1-10
This content is part of a series Mahubiri, in .

VUNJA VIZUIZI

Date preached October 12, 2025

TWEKA KILINDINI
Luka 5:1-10

Mashua
Petro
nyavu
bahari/ziwa
samaki

Aya hii sio ngeni lakini kuna vitu ambavyo hujawahi kuviona kwenye aya hii hii Mungu ameniambia nikwambie

Yale ambayo Mungu anataka kufanya maishani mwako utahitaji usaidizi

Anataka kukupa kitu kikubwa kuzidi mashua yako

Waliokuja kumsaidia nao mashua zao zilianza kuzama

“Simoni Petro alipoona hivi alianguka akamsihi akisema ondoka kwangu maana mimi ni mwenye dhambi”

Somo letu ni “vunja vizuizi”

Kwa muda nilioishi nikihudumu katika Neno nimeshuhudia watu wengi wengi wakiamini na kubatizwa lakini wengi wao wanakosa maisha tele

Kuwahubiria na kuwabatiza sio mwisho wa kazi ya mwinjlisti kwa sababu kuwabatiza na kuwaacha wamekwama bila uelewa wa neno unakuwa hujawasaidia kuvuka vizuizi vinavyoweka ukomo wa maendeleo yao. Ni kama na wewe unasaidia wakwame

Wanapaswa kujua wao ni nani katika Bwana na jinsi ya kuzifurahia ahdi za Bwana

Nimegundua kwamba mara nyingi anachoamini mtu ni kipenyo kidogo cha jambo zima lakini kibaya zaidi anakuwa ameaminishwa kwamba hicho ndicho kitu kizima anachopaswa kujua na kuishi nacho

Ukweli kabisa ni kwamba mbali na baraka za rohoni pia kuna baraka za mwilini kwa watu wa Mungu na wengi wetu tunafanikiwa kupata za rohoni bila zile za mwilini

Ndani ya mtu kunakuwa na mifumo ya imani ambayo inaweza kukataa fursa ambazo Mungu ametupa

Biblia inasema Simoni alikuwa anaosha nyavu

Mifumo yake ya imani iliyojengwa juu ya mazoea na desturi ilikuwa imemwambia hakuna samaki

Mifumo hiyo hiyo ilimfundisha kwamba samaki wanapatikana usiku

Walikuwa wamefanya kazi usiku kucha bila kupata kitu

Mifumo ya imani ilimwacha akiwa amekikatia tamaa alichokihitaji

Kwamba usipopata usiku hupati kabisa

YESU ANAKUTANA NA WAVUVI WALIOKATA TAMAA
Yesu alipokutana na wavuvi waliochoka walikuwa wanaosha nyavu jambo ambalo ni uthibitisho wa kukata tamaa

Na leo anakutana na wewe unaosha nyavu umekata tamaa lakini pia umechoka

Nataka nikuonyeshe kwamba Yesu aliyemshangaza Simoni atakushangaza na wewe

Yesu atakuonyesha kwamba mifumo yako ya imani imekuwekea ukuta

Imekuwekea ukomo

Kuosha nyavu kulimaanisha kwamba hawawezi kuendelea kabisa

KUliamaanisha hawana matumaini tena

Umeona vyema kusali tu, umeona uishi tu kuliko kuendelea kuumia na kuchoka

Umeridhika na mashua isiyo na samaki jambo ambalo kwa simoni lilimaanisha hakuna biashara siku hiyo

Hakuna kipato siku hiyo

Unapopitia hali hiyo popote ulipo katika shughuli zako za kujipatia riziki unafika hatua ya kujidanganya ili ujifariji kwa kusema haukuwa mpango wa Mungu

Usihofu, hata Simoni alifikiri hivyohivyo ndio maana hakuonekana kupambana

Hakuonekana ana huzuni

Hakuana ni jambo baya, maana limezoeleka maishani mwake

Simoni alikuwa anaosha nyavu:

Kuosha nyavu kuna maanisha hakuna atakayekupenda

Kuosha nyavu kunamaanisha huwezi kuongeza elimu tena

Kunamaanisha umeamua kwamba huwezi kwenda mbele

Kuosha nyavu ni kuzikatia tamaa ndoto zako na kudhani kwamba jitihada zako zote zilikuwa kwa ajili ya usiku

Na kwa vile hakuitokea kama alivyodhani, kama alivyozoea

Aliacha kuvua akawaanaosha nyavu

Yuko hai lakini ameacha

Anapumua lakin ameacha

Utashangazwa kukutana na watu wanaopumua alakini wamekufa

Wana make up, wamevaa suti, wavaa vizuri, lakini wameacha

Wanakuja kanisani lakini wameacha

Wameacha!

Wanapeana maua lakini wameacha

Wanapika chakula lakini wameacha

Watu wanaweza kuacha huku unaowaona sebuleni, huku unawaona kanisani

Huku unawaona nyumbani

Watu wanaacha huku wanaendelea kutoa sadaka

Simoni aliacha kuvua lakini alitoa mashua yake

Kuacha ni kujiondoa bila kuondoka

Moyo wa Petro ulikuwa umevunjika na alikuwa anaosha nyavu

Aliacha lakini bado alikuwa anafanya usafi kanisani

Bado alikuwa anapamba kanisani

YESU ANAVURUGA MIFUMO YA IMANI YA PETRO

Hata kama Petro alitaka aendelee kuosha nyavu zake Yesu alitaka asiendelee kuosha nyavu

Lile linalokufanya uwe na amani nalo ndilo linalokufanya uwe umeacha hata kama tunakuona

Kuna watu wameacha kazi hata kama wako kwenye vituo vya kazi

Kwa sababu hawajafikia malengo

Wanapukuta meza lakini wameacha

Wanafuta madirisha lakini wameacha

Wanaenda kazini lakini wameacha

Kuna watu wameacha uinjilisti hata kama unawaona na Biblia

Wanachofanya ni kupukuta Biblia

Ni kusafisha kanisa

Wamekata tamaa baada ya kufanya kazi bila kupata samaki

Samaki ndio malengo! Samaki ni lengo la uinjilisti

Umeshindwa kwenda mbali peke yako

HUjapata samaki lakini wapo

Yesu anayetosha kwenye pochi ni tofautina Yesu wa kilindini

Tuna Yesu ambaye ni mvunja nira na kongwa

Yesu anakuja nyumbani kwako

Anakuja kwenye uchumi wako

Anakuja kwenye elimu yako

Anakuja maishani mwako

Anataka kutumia mashua yako ili iwe mimbari yake kuwahubiria watu

Baada ya hapo kila jambo ulilodhani limefika mwisho litaanza upya

Mungu anataka ujue kwamba mashua ni maisha yako,

Mashua ni biashara yako

Mashua ni elimu yako

Mashua ni familia yako

Una mashua ambayo ina ukubwa uliosababishwa na mazoea, ukimpa Yesu aitumie itajaa samaki

KIPELEKE MBALI KIDOGO NA PWANI

Kisiwe kilipokuwa

Kisiwe mbali na watu lakini kisiwe mahali walipo watu

Yesu hakuingia kwenye mashua na kuanza kuongea na watu, alitaka kuwe na juhudi ya Petro

Sio tu Yesu anakuja kwako na kuingia kwenye maisha yako na kuanza kuyatumia

Sio anaingia tu kwenye biashara yako na kuanza kuitumia

Sio anaingia tu kwenye utumishi wako na kuanza kuugeuza kuwa madhabahu

Bali anataka uyasogeze maisha yako mahali ambapo patafaa yeye kuongea na watu

Kuna jitihada inahitajika kabla maisha yako hayajawa madhabahu,

Kabla miili yetu haijawa dhabihu kuna jitihadi ya positioning

Jambo ninaloliona hapola uhakika ni kwamba Yesu anaweza kuingia maishani mwako na ukawa naye

Lakini kama unataka Yesu aongee na watu ni lazima ufanye alichofanya Petro-positioning

Mwanzo wa uamusho kwa Petro ni pale anapoacha kuosha nyavu na kurudi kwenye mashua ili aisogeze ili Yesu aitumie

HIli ndilo lengo la mimi kukualika ili uache kuosha nyavu, urudi mashuani, uendeshe sio kwenda kuvua samaki wa biashara bali Yesu aitumie mashua yako kwa namna ambayo sio malengo ya mashua yako

Sio malengo ya waliotengeneza mashua

Akutumie nje ya malengo ya wazazi wako

Nje ya malengo yako

Akutumie kwa malengo yake huku ukiwa umekosa malengo yako

Haikuwa rahisi!

Wengine mngesema mashua nimekupa isogze mwenyewe mimi ni mechoka

Usinisumbue sijalala usiku kucha

Ilihitaji utii nyakati ngumu

Ilihitaji utii nyakati una njaa hujala

Ilihitaji utii nyakati ambazo watoto wako walitegemea urudi na samaki na hujarudi na Yesu anataka akutumie kuisogeza mashua

Kwani ungekubali kuisogeza mashua kwa ajili ya mtu usiyemjua na hajakwambia anataka aitumie kwa ajili gani

Lakini kwa nini aliichagua mashua ya Petro?

Hata mimi ningejiuliza hilo swali kabla sijaamua kukataa aua kuisogeza mashua

Petro anadondosha nyavu zake na kwenda kuendesha mashua kwenda anakotaka Yesu

Toa ulicho nacho kwa ajili ya Yesu, maisha yako, ajira yako, mali zako, elimu yako, muda wako, ujuzi wako, nguvu zako

Alichofanya Petro ni Uamusho!

Acha kujilaumu

Acha kuongelea ulivyoshindwa

Acha kuongelea ulivyopata hasara

Acha kuongelea nguvu uliyotumia ambayo haikukupa chochote

Unapoosha nyavu unawaza ulivyoshindwa sio unavyoweza kupata

Hayo yamepita

“Hata imekuwa mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kkiumbe kipya…”

Huwezi kubadilisha lililotokea

Yaliyopita yamepita

Usisishi leo huku unafanya mazoezi jana

Jana yako isiibe leo yako

“Bwana tumefanya kazi usiku kucha lakini hatukupata kitu”

Yesu anasema tweka kilindini Petro anazungumzia walichofanya usiku

Imani inamwambia ukikosa usiku mchana huwezi kupata.

Yesu anasema, Petro anasema

Yesu anasema, Mazoea yanasema

Yesu anasema, kukata tamaa kunasema

Ni kama anasema haiwezekani

Oh Haleluya! Naona jambo lingine hapa,

Kilindini ndiko mahali ambako wavuvi wengi hawaendi lakini ndiko samaki wanakokuwa nyakati za mchana

Kilindini mashua inazama

Kilindini hakujazoeleka

Kilindini kuna samaki

Mwambie jirani yako, utakosa samaki kwote lakin Yesu anasema sio kilindini

Baada ya biashara ya Petro kuwa madhabahu

Baada ya maisha ya Petro kuwa madhabahu

Baada ya uchumi wa Petro kuwa madhabahu

Na umati ukiwa ufukweni, Yesu alihubiri na watu waliona heri kuzimia na njaa kuliko kukosa kumsiliza Yesu

Mwite leo aketi maishani mwako

Alipomaliza kuongea na watu, na hapa hatujaambiwa aliongea nini na watu kwa sababu nguvu ya aya ipo kwenye matemdo yaliyotokea

Alimwambia simoni ” Tweka kilindini”, Shushueni nyavu

Nyavu zilizooshwa?

“Imani ni kuwa na hakika na mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mabamo yasiyoonekana” Waebrania 11:1

Kurudisha na kuzishusha nyavu kilindidni kulimaanisha zitahitaji kuoshwa tena.

Ilihitaji imani!

“Lakini Pasipo hiyo imani haiwezekani kumpendeza…”

Ilihitaji utii

“Tweka kilindini”

Bado hujaelewa,

Yesu anasema ondoka kwenye maji machache zamisha nyavu kwenye maji mengi

Sema “kilindini”

Mwambie ulipo hapana kina cha kutosha kupata samaki. Maisha yako yamezoea maji madogo tweka kilindini

Ukitaka kupata maarifa ya Mungu ondoka kwenye maji madogo tweka kilindini

Kinachofanya uwe hivyo ulivyo sio bahari kutokuwa na samaki bali ni wewe kutompa Yesu maisha yako ili akwambie walipo samaki

NI kwa sababu hujaenda kwa kina

Umetumia nguvu nyingi, umetumia mali nyingi, umetumia muda mwingi kwa akili ya mazoea

Jiandae kuona anachoweza kukupa Yesu

Shetani alilenga kukutesa

Shetani alilenga usihindwe kutunza watoto wako

Shetania lilenga kukuhuzunisha

Pengine Petro alihitaji samaki siku ile kuliko nyingine yoyote kwa ajili ya familia yake

Ndio wakati ambao alikosa samaki

Hata kama sina hakika

Hata kama sijawahi kwenda

Hata kama kunatisha

Hata kama nyavu zitachafuka

“kwa neno lako Nitazishusha nyavu”
Warumi 10:17 “imani chanzo chake ni kusikia na Kusikia huja kwa neno la Kristo”

Luka 6:46-49

Tweka kilindini!

Kilindini ni kina kirefu

Lazima useme nimechoka kuishi ndani mipaka, ndani ya vizuizi sasa najianda kwenda kwenye kina

Naendaa kuzishusha nyavu

Naenda kwenye viwango vipya

Hujui kwamba sababu ya Mungu kukupa ulivyo navyo ikiwa ni pamoja maisha yako ni kwa sababu anataka viwe jukwaa la injili

Heshima ya maisha yako iwe jukwaa la injili na sasa unahangaika na matatizo na matatizo hayako kwenye kile unachofanya

Matatizo yako ndani yako

Ukimsikiliza Yesu, Ukimpa YEsu mashua yako aitumie

Kila kitu kitabadilika

Kila kitu kwenye maisha kitabadilika

Tweka kilindini wakati watu wanadhani utaosha nyavu

Wanapodhani utaacha tweka kilidini

Wanapodhani utajiua tweka kilindini

Wanapodhani watoto wako watakufaa njaa tweka kilindini

Mwambie jirani “nashusha nyavu kilindini”

Usipozisha nyavu kilindi huwezi kupata samaki

Ukiogopa kufa kilindini huwezi kupata samaki

Twende kilindini au ubaki ufukweni

Twende kilindin au uendelee kuosha nyavu huku umeacha

Wengine wanasema sijawahi kwenda kilindini, lakini hilo haliondoi kilindi kuwa na samaki unaowakosa kwenye maji madogo

Yesu amekupa kibali cha kwenda kilindini, nenda samaki wapo

Kilindini kwako ni wapi?

Labda ni kijiji fulani, labda ni mkoa fulani, labda ni tv fulani, labda ni redio fulani, labda ni ofisi fulani, labda ni chuo fulani, labda ni shule fulani

Sijui Yesu anakutuma kwenda wapi lakini ninachojua kilindini kuna samaki

Kwa kawaida nyakati za mchana huwezi kuvua lakini Yesu akisema nitaenda kilindini

Mazoea yanasema lile ni kabila gumu lakini Yesu akisema nitaenda

Mazoea yanasema kule ni ghrama kuishina familia yangu lakin Yesu akisema nitazishusha nyavu

Mazoea yanasema kule sijaozoea laini Yesu akisema, nitaenda

Moyo wangu unasema siwezi lakini kwa neno la Bwana nitaizishusha nyavu

Shetani anapokukatisha tamaa kwamba haiwezekani,

Umepodhani majira na nyakati zimepita

Yesu anasema samaki wapo

Unajiuliza kwanini, unajiuliza inawezekanaje?

Ni kwa sababu simoni anamiliki mtumbwi lakini Yesu anamiliki samaki na anajua walipo

Simoni ana mtumbwi lakin Mungu ana bahari

Yesu anajua walipo samaki unaotafuta usiku kucha

Wakati ambao wenzio wanaosha nyavu na wengine wamelala vimvurini ndio wakati wa kumsikiliza Yesu anataka kukutuma wapi

Wengi wanaangalia wasiofanya kazi, wanaolala, wanaoosha nyavu na wao wanaosha nyavu

Vunja sheria ya mazoea!

Sheria inasema samaki wanapatikana usiku Yesu anasema usiku ni wakati wa kazi za shetani

Shetani anajua unajua kwamba samaki wapo usiku na hivyo anapiga usiku

Yesu anasema samaki sio tu wapo mchana lakini wapo kilindini

HUjachelewa kwend akuanzisha kusanyiko

HUjachelewa kufungua huduma

Unachochelewa ni kufika kilndini

HUjachelewa kuanzisha biashara bali biashara yako imeshusha nyavu kilindini?

HUjachelewa kuanza maisha, lakini je uko tayari kwenda na Neno la Bwana!
Jiandae kwenda kwenye kipenyo kipya

Kazi yako ni kushusha nyavu, kazi ya Mungu kukupa samaki

Kazi yako ni kumpa Mungu ulicho nacho, Kazi ya Mungu ni kukwambia kwa kwenda kuzindua upya maisha yako

Navunja vizuizi na mipaka uliwekewa maishani mwako

Navunja mipaka iliyokubakisha ulipo

Najunja vizuizi vinavyosimama kati yako na Neno la Bwana

Nafungua malango yaliyofungwa maishani mwako

Mipaka imezoeleka mpaka imekuwa maisha yako

Imezoeleka mpaka imekuwa wewe

Hadi umejikuta wewe ndio mipaka yenyewe

Hadi unaitetea

Umekata tama kiasi cha kutumia muda wako kuosha nyavu

Umeacha kuvua unaosha nyavu, nakwambia acha kuosha nyavu anza kuvua

Mungu anataka usiache ulichoacha
Mungu anasema acha unakataa kuacha, ulichochelewa kuacha

Mungu anasema rudi ukavue

Uende unakosita kwenda

Uende unakoogopa kwenda

Huu sio wakati wa kuosha nyavu

Huu ni wakati wa kuzishusha nyavu

MASHUA YA PETRO ILILINGANA NA MAZOEA

Nimewahi kuona majengo yanayotosha watu 15. Wengine wanasema kubwa la nini?

Walipozishusha nyavu, samaki walikuwa wengine hata nyavu zikataka kukatika

Walipoomba msaada kwa wengine mashua zao zikataka kuzama

Watu wanawaza na kutenda sawasawa na mazingira. Petro na wengine walikuwa na nyavu zinazotosha samaki walizozoea

Nyavu ulizonazo hazitatosha na jambo pekee unalopaswa kuomba kwa Mungu ni kuomba akili. Kuomba mabadiliko ya akili

Hili jambo lenye uhusiano na nyavu,

Wanapokutana na Yesu alikuwa wanaosha nyavu

Walipoingia kwenye mashua hawakukagua ukubwa na uimara wa nyavu

Kwanini Petro hakushusha nyavu imara

Kwa nini hakushusha nyavu kubwa

Kuridhika kwako kunatangulia mbele ya Neno la Bwana

Mazoea yako yanakuwa mbele ya ahadi za Mungu

Petro hakujua kama nyavu zitatka kukatika

Hakujua kwamba atahitaji msaada wa wengine

Kwa sababu hajawahi kufikiri hivyo

Aliziamini nyavu kuliko kuamini Neno la Bwana

Hata kama alisema kwa Neno lako nitaenda

Alijua suala ni kushusha nyavu

Alijua kushusha nyavu kilindini ni kushusha nyavu

Kushusha nyavu kilindini kumaanisha kukagua nyavu ulizonazo

Kulimaanisha kutathimini rasilimali alizonazo kama zinaendana na kilindini

Alitumia nyavu za maji madogo kwenda kilindini

Shusha nyavu!!!

Kilindini kuna samaki wengi sana wanaosubiri utii neno la Bwana

Kilindini ni tofauti na ulipozoea na kuzoeleka

Utii ndio utakaovunja mipaka

Mipaka ya mafanikio ya Petro haikuwa baharini

Mipaka ilikuwa kwenye nyavu na mashua

Hakuna anayeenda kuvua na amshua ambayo anategemea umwombe akusaidie kubebea samaki zako

Kila anayeenda kuvuaa anaenda na chombo kinachotosha na anaenda nyavu inayotosha

Maisha ya Petro yalitosheka na samaki walioendana na nyavu alizokuwa nazo

Hatuwezi kusema Petro hakumtii neno la Bwana! Angalau anatofautiana na wengi wetu

Alitoa mashua itumiwe na Yesu

Alikubali kumpeleka Yesu mahali pa kuhubiria

Warumi 10:14-15

ìWataendaje wasipopelekwa?

Angalau Petro alihatarisha maisha yake (mashua) kwenda sehemu ambayo hajawi kwenda na angezama pia

Lakini alienda

Angalau alikuwa na imani ya kubeba nyavu akiamini atavua

Lakini anafanana na wengi wetu hasa watumishi wa Mungu kwa kwenda kilindini na tabia(nyavu) za maji madogo

Nyavu ndizo hunasa samaki na tabia zetu ndizo hunasa watu waje kwa Kristo

Mungu amehifadhi samaki wengi kwa ajili yako kama uko tayari kwenda

Mifano ya Mungu Warumi 11:4

ìKwanza utanulizeni ufalme wa Mungu na haki yakeî

Wengi hatuamini hii aya hata kama tunaisoma ndio maana nimesema Kuna uwezekano ukawa huamini unachoamini

ìNa hayo yote mtazidishiwaî

Kuzidishiwa kwa namna ya kukatika nyavu

Kuzidishiwa kwa namna ambayo utahitaji msaada

Mtangulize Mungu katika uchumi wako

Mtangulize Mungu katika kazi zako

Mtangulize Mungu katika kilimo chako

Mtangulize Mungu katika biashara zako

Ukifanya hivyo tii neno la kwenda kilindini

Utakata nyavu

Luka 6:38

Petro na wenzake mashua na nyavu zao hazikutosha

Na Mungu ameniambia nikwambie kwamba samaki hawakuisha kilindini ila Petro mahitaji yake hayakufanana na mashua na nyavu alizo nazo. Jambo hili lilimfanya aache samaki ambao angewahitaji kesho

Kuwa makini na kibebeo cha majibu ya maombi unayomwomba Mungu

Mahali huduma inaenda itahitaji wasaidizi

Mahali maisha yanaenda utahitaji wasaidizi

Mahali biashara yako inaenda utahtaji wasaidizi

Lakini kwanza ufalme wa Mungu kisha Tii na hayo yote Ö..

Unahitaji mashirikiano

Kwa sasa unafanya mwenyewe kila kitu kwa sababu hujatweka kilindini

Kila anayechukua neno hili popote ulipo unapaswa kuwa na mpango mkakati wa kuhimili uzito kiwango kinachozidi kiwango ulicho nacho sasa

Utahitaji vitendea kazi

Nawaona wengine wakiwa wainjilisti wa mikoa, wainjilisti wa Taifa, Wainjilisti wa kimataifa

Nawaona wengine wakiwa wafanyabiasha wa kimataifa

Tweka kilindini

Lakini unahitaji passpot kuliko unavyohitaji Nida

Matokeo ya kilindini huwezi kuyabeba kama ulivyozoea kwa sababu yapo kinyume na mazoea na mifumo ya imani

Kwa sababu kilindini kunazidi mifumo utahitaji kuandaa mifumo

Petro alivua samaki wangapi?

Aliacha samaki wangapi?

Lakini Petro alikosa samaki wangapi kabla ya pale

Samaki hawa wote walikuwa wanaishi palepale Genezareti

Walesamaki hawakuumbwa siku ileile

Walikuwepo siku zote

Hivi unajua umekosa mangapia miaka yote hii kwa kushindwa kumpa Mungu maisha yako ayatumie

Kwa kushindwa kumepeleka Yesu akahubiri vijiji mbalimbali

Kwa kushindwa kutii?

Ni kweli unamwini Mungu

Ni kweli umebatizwa

Ni kweli ni kiongozi kanisani kwenu

Lakini inawezekana huamini

ìBwana nisaide kutokuamini kwanguî

Unapoosha nyavu, mashua hujaiosha-Mpe Yesu itafaa tena

 

Unapoosha nyavu unadhani ndio basi

Kuna samaki wengi kilindini

Wengine mali mlizonazo zinawazuia kwenda kilindini

Ndugu mlionao mmewazoea sana hata hamuendi kilindini

Nyumba uliyojenga hutaki kuiacha ili ukahubiri vijijini

Watoto ulionao wamekuwa kizuizi cha kwenda na hivyo upande wa pili wamekuwa kizuizi cha Baraka zako

Samaki wapo kilindini

Mungu anataka kukuonyesha kwamba yapo mengi usiyoyajua

Mwambie jirani nimepewa kibali kwenda kilindini!

Mshauri jirani yako abadilishe nyavu na mashua

Kilindini kuna samaki

Una kibali cha kuvua samaki mchana

Una kibali ambacho wengine hawana

Kibali kinakufanya uvue samaki wakati usio kufaa maana wakati unaokufaa ni usiku

Anachotaka kukupa Mungu kwa kawaida hakikupaswa wakati huu wa huduma yako, wakati huu wa umri wako

Ukiachana na mapokeo, Mungu atakufungua

Onyo ni kwamba mapokeo na mazoea yatakufanya ukose samaki ambao Mungu amekuandalia

Umeitwa na Mungu uende kilindini na sio kwenye maji ya ugoko

Huwezi kupata maarifa ya kina ya neno la Mungu kwenye maji madogo

Huwezi kupata mafanikio kwenye maji madogo

Huwezi kuvua samaki wa kukutosha kwenye maji madogo

ILI UPOKEE ALIKUANDALIA MUNGU UKUBALI HASARA

Nyavu zilitaka kukatika-usidhani hazikuonyesha nyufa

Mashua zilitaka kuzama-usidhani hazikuanza kuzama

ìatakayepoteza maisha atayaonaî

Wafil. 3:7-9

Ukubali mabadiliko maishani mwako

Kuna mambo yatavunjika

Kuna urafiki utavunjika kutoka na uzito wa utukufu wa Mungu maishani mwako

Utalazimika kuvunja imani ulizozoea

Hii ni zaid ya samaki

Biblia ya King James inasema walivua ìmultitudes of fishî. Yaani lundo la samaki mst. 9

Nasema ni zaidi ya samaki kwa sababu jicho la ndani Linaona mambo mawili

1. Biashara-Uchumi-mafanikio-rasilimali-kipato
Biashara ya Petro inaenda mbali na upeo wa kibindamu na mazoea
Kujaza mashua yake
Kujaza mashua za wenzake hadi kila kiti chenye uhusiano na Petro kilipojaa.
2. Uinjilisti

Kwa hiyo unaposoma hapo usisome habari ya samaki tu bali kuna biashara na uinjilisti

Walipoegesha vyombo vyao Biblia inasema walimfuata Luka 5:10-11
Mathayo 4:16

PETRO KUKUTANA NA YESU HAIKUWA MATOKEO YA UTAKATIFU WAKE

Luka 5:8
ìondoka kwangu maana mimi ni mwenye dhambiî

Samaki hawakuwa thawabu ya utakatifu wake bali samaki walikuwa thawabu ya utii wake

Sema utii unalipa!

Alitoa mashua

Alimpeleka YEsu

Alimtii Yesu

ìKwa neno lako nitazishusha nyavuî

Yesu alimbariki Petro na biashara yake na akamwahidi kumbariki zaidi na zaidi

ìTangu sasa utakuwa unavua watuî
Ngoja nikupe siri iliyoko hapa
Mazungumzo haya yanafanyika mwanzoni mwa huduma ya Bwana Yesu na Mwishoni mwa huduma ya Bwana Yesu

Na nyakati zote mbili Petro anakutwa amekata tama

Nyakati zote mbili Petro anatumwa kuvua samaki

Na nyakati zote mbili anakutwa hajapata kiti

Mwishoni mwa huduma ya Yesu, Petro anarudi kuvua samaki kwa sababu Yesu amesulubiwa na ameshakufa

Yohana 21:1-12
Yesu alipokuwa akitembea pembezoni mwa bahari baada ya kufufuka kwake
Na mazungumzo yanafanana kwa kiasi kikubwa

ìWalimwambia tumefanya kazi usiku kucha lakini hatujapata kituî

Yesu aliwaambia tupeni jarife upande wa kulia wa mashua

Kutokana na wingi wa samaki waliopata ulimsaidia Petro kukumbuka
Tukio la kwanza

Ni kama alifika duara ya maisha yake ilipoanzia

Lakini kwa sasa haikuwa kilindini

Kumwelewa Yesu maishani mwako kunakusaidia kujitambua maishani mwako

Wengine wanamwelewa Yesu lakini hawajielewi wenyewe

Wengine wanawaelewa wengine lakin hawajielewi wengine

Safari hii Petro hakungoja afike na samaki ufukweni

Alisema hatafanya makosa aliyofanya mara ya kwanza

Alijisemea moyoni ìhaa kama amenibariki kwa samaki, hili sio jambo la samakiî Ni jambo la uinjilisti

Hilo sio jambo la uchumi tena bali ni la uinjilisti maishani mwako

Ni jambo la kupata kifungua kinywa ukahubiri ni jambo la Bwana!

Petro akaruka na kuanza kuogelea kwenda kwa Yesu

Kuna wakati inabidi uache biashara unapofika muda wa Bwana

Kwana wakati inabidi ufunge ofisi unapofika muda wa Bwana

Kuna wakati inabidi uondoke numbani unapofika muda wa Bwana

Safari hii aliacha mtumbwi ukiwa umekwama na samaki 153
Najiuliza ile mashua ilikuwa ni nyingine au ni ile ile aliyokuwa nayo mwanzo?

Safari hii hakupanda mashua

Watu waliokata tama wana kawaida kurudia walichokuwa wanafanya mwanzo

Waliokata tama wana kawaida kuwarudia marafiki wa zamani

Tusiache kuwatembelea na kuwakumbusha

Tusiache kuwapenda

Biblia inasema safari hii Petro alikuwa uchi

UKIENDA KWA YESU ULICHOACHA UNAPATA KWA YESU

Alipofika alikuta Yesu anabanika samaki-Wakati wanaenda kuvua samaki Yesu alipata wapi samaki?

Petro aliachana na samaki wa kwenye mashua lakini hakukosa samaki

Faida ya kwenda kwa Yesu

Faida ya kumkimbilia Yesu

Unaacha samaki wabichi unakutana na samaki aliyeiva! Haleluya!

Unapoacha samaki wabichi ni lazima usijua kama kuna samaki walioiva ufukweni ili iwe thawabu ya imani

Petro safari hii alipata thawabu ya imani

Zaburi 23:5
ìBwana anannidalia meza mbele ya watesi wanguî

Utatembea ndani ya Baraka zilizoandaliwa na Mungu kwa ajili yako

Yesu alijua Petro atafanya maamuzi sahihi ndio maana akawa anaoka samaki wakati Petro anaogelea

Fanya maamuzi sahihi leo

Mungu anakuandalia kifungua kinywa, chukua hatua!

Vunja mipaka

Vunja mapokeo

Kwa mara nyingine Petro anahatarisha uhai wake

Mara ya kwanza alihatarisha kwa ajili ya samaki na sasa anahatarisha kwa ajili ya Yesu
Anaogelea akiwa uchi

Mwambie jirani yako ìutapata mengiî Marko 10:28-52

Baada ya siku ile hatumwoni Petro akiwa na mashua kwa ajili ya samaki

Petro alikuwa ameliewa kusudi kuu ambapo mashua ilikuwa ni mafunzoni tu

Kama unanielewa, ni hivi;

Usiomboleze kwa ajili ya mambo uliyopoteza

Chochote unachowekeza kwa Mungu,kipawa, mali, muda havijaiva, Mungu anakuandalia samaki waliookwa ufukweni

Ninakuombea kwa sababu najua adui alikuwa anaogopa sana kwa wewe kupatana neno hili

Anaogopa kwa sababu Mungu anaenda kukufungua

Alikuzuia kwa njia nyingi

Alikuwekea majaribu ili usifike kilindini

Ili usifike ufukweni

Anakuzuia usifanye kazi ya Mungu ili urudi kwenya uliyozaliwa nayo

Na hiy o ndiyo njia pekee ya kuzuia utii

Utii ni kufanya niliyoagizwa na Bwana

Mungu amekuandalia Baraka, kama unadhani hili ni somo tu ni shauri yako lakini wengine wanachukua kama ujumbe wa Bwana maishani mwao

Mungu anataka kuyatumia maisha yako kama jukwaa

Tatizo la kwanza hatuko tayari maisha yetu yawe jukwaa

Pili hata tunapokuwa tayari nyavu zetu ni ndogo kuliko ufalme wa Mungu

Ni sadaka gani unaweza kumpa Mungu zaidi ya maisha yako?

Ni alama gani unaweza kuiweka kwenye kanisa kama sio maisha yako na mali zako

Baadhi yenu mna moyo kuweka alama, wa kutoa sadaka lakini hamkuwahi kubahatika hata kuwasaidia wazazi wenu hadi wameondoka duniani na unaomba wangekuwepo ingeweka alama maishani mwao ingawa sio kuwalipa

Hapa kuna Mungu ambaye unamhitaji kuliko anavyokuhitaji lakini anakupenda kuliko unavyompenda

Mungu amekupa fursa ya kumpa maisha yako

Fungua mipaka iliyofungwa maishani mwako Katika jina la Yesu Kristo!

Navunja ukomo uliowekewa!

Endelea kuomba, Mwambie Mungu akuonyesha maeneo yaliyofungwa maishani mwako

Chuki, wivu, uadui vinaua kesho yako

Jinsi unavyojidharau unaua kesho yako

Jinsi usivyojiamini unasababisha watu wasikuamini

Kama sikwambii haya kwa sababu niko hapa basin i kwa sabab Mungu ameniambia nikwambie

Kama unaweza kulipokea neno hili sasa lipokee

Wengine wamelisikia lakini hawajasikiliza

Wamelitazama miaka mingi lakini hawaliona

Lakini kama umeliskia na kuliona ni kwa sababu tu roho amefungua masikio na moyo wako ulipokee

Na hiyo ni Baraka

Tenda sasa sawa sawa na neno hili

Uwe tayari kumpa Mungu maisha yako na mali zako

Ili ninapoomba niifunike sadaka yako

Ni muhimu sana ili usirudi kuvua samaki tena

Ni muhimu ili usirudie kuwa mwongo mwongo tena

Ni muimu ili usirudie kuwa mjanjamjanja tena

Kwa sababu Mungu atakuvusha kutoka imani hata imani

Kutoka utukufu hadi utukufu

Na ataendelea kufanya mambo makuu ndani yako na kukupeleka katika viwango vya juu katika kumjua kwa ajili ya kusudi lake mwenyewe

Mwambie jirani yako

ìMungu hajaishia hapa, hajamalizana na wewe bado

Acha kuosha nyavuî
Yesu atageuza maishua yako kuwa jukwaa

Na hiyo itabadilisha mweleko wa maisha yako

Akikaa kwenye mashua yako kila kitu kitabadilikaî

Inua mikono niombe na wewe

ìAsante Yesu, mimi mtumwa tu bali wewe ndiye uliye na kusudi la maisha yangu

Kusudi la kuzaliwa kwangu, kusudi la kuumbwa kwangu

Kusudi la kuokoka kwangu

Nakupa kila eneo la maisha yangu

Siwezi kufungua mipaka bila wewe kwa sababu wewe ndiye ufunguo

Naomba unifungue niishi maisha uliyokusudia niishi

Nisaidie nitimize kusudi lako maishani mwangu

Naminiuone utukufu wako na sio heshima yangu

Ili ulimwengu ujue kwamba wewe ni baba yetu

Katika Jina la Yesu Kristo, Amen!

In series Mahubiri