All Sermons
Bible Passage 1Wakor. 6:19
This content is part of a series Mahubiri, in .

MKATE WA MBINGUNI

Date preached June 1, 2025

Ni muhimu sana kufahamu somo hili linalohusiana na mkate na hema ya kukutania kwa sababu nafahamu kwamba ni vigumu kumfahamu Yesu na kulifahamu neno kama huelewi hema ya kukutania.

Wengi wanafahamu hadithi za Biblia lakini wakati fulani ni vigumu kujua zina maana gani

Wote tunajua Yesu alienda msalabani lakini unaweza usijue kwa undani kwamba damu yake ilikuwa ni muamala wa kukununua

1Wakor. 6:19

Kwa hiyo unajikuta unatumia maneno kama ukombozi, lakini hufikirii kwa undani maana yake

Ni hadi unapoenda kwenye hema ndipo utaona damu juu ya madhabahu

Ndipo unapotambua kwamba Yesu alipopaa ilikuwa muhimu apae kupita mawingu hadi Pa patakatifu pa PatakatifuI have done it

Hema ilijengwa jangwani mwaka mmoja baada ya pasaka. Mwaka mmoja tangu waisraeli watoke Misri

Mungu alimwambia Farao waachie watu wangu wakaniabudu. Ujenzi wa hema ulikuwa ndio mwanzo wa kusudi la Mung kuwatoa Misri

Ni lazima ufahamu kwamba kuanzia Mwanzo na kuendelea anachotaka Mungu ni kuwa na mwanadamu

Mika 6:8

Aliweka bustani ya Edeni ali awe na mahali pa kukutana na mwanadamu

Alituumba kwa mfano wake ili tuwe na ushirika naye sio dini

Watu wengi wana dini lakini hawana ushirika na Mungu. Mungu anataka tuwe na ushirika naye

Aliiumba dunia ili apate kukaa nasi kwa ushirika

Alipofika bustanini na akaona mwanadamu hayuko kwenye ushirika akasema Adamu uko wapi?

Katika somo hili tunaangalia Kutoka 25:8

Yohana 14:1
Waebrania 9

Kwa kuwa hamuwezi kupanda juu basi Mungu aliwambia wana wa Israeli kwamba yeye atashuka na kukaa kati yao

Aya nyingine ninayotaka tusome ni Zaburi 91:1,9

Somo hili litasaidia kukua kama Mtumishi na kuhani.

Tukiacha kwenda kanisani kama kikundi cha kufa na kizikana na tukaanza kuja kanisani kama mahali pa kujifunza Neno la Mungu tunajifunza kwa umakini

Zingatia tofauti tunazoziona katika aya hizi;

Kutoka 25:8 Nijengeeni hema nipate kukaa kati yenu

Zaburi 91:1 Mungu akikaa kwenye hema haina faida kama wewe hukai naye

Kuna mambo unayapata kwa kutembelea na kuna mambo makubwa unayapata ukikaa naye

Unatakiwa kumtembelea Mungu unapokuwa na shida kwa sababu faida halisi zinapatikana unakaa naye

Sasa tuone mstari wa 9

Hiyo sio ahadi kwa wanatembelea kanisa. Ni ahadi kwa wakaaji, walio imara.

Unaweza kumshangilia Mungu ukiwa unaumwa?

Ukiwa umefilisika?

Ukiwa kwenye mgogoro?

Kumbukumbu 29:29

Bwana huwapa siri wale wamchao

siri hizo hawezi kukupa hadi ukae naye

Nikiwa kwenye hali mbaya nikae, Nikipitia wakati mgumu nikae, Sitambelea Mungu ila nitakaa

Wana wa Israeli walijenga hema zao kwa kuizunguka hema ya kukutania ilikuwa katikati. Mungu alikaa katikati yao

Kabla ya kujenga hema walikuwa
wanakaa chini ya wingu na nguzo ya moto
alikaa kati yao hema ilipojengwa (anakaa karibu zaidi, sio winguni, bali aridhini)
Wakati watu wengine wako hemani, wanaume walikuwa wanaingia kwenye behewa ili wamkaribie Mungu

Kuna watu hapa wako kwenye behewa. ni sawa, usihofu maana hata somo letu sasa tuko kwenye behewa

Behewa. Ufunuo 11

Hapa ndip palikuwa na Madhabahu ya shaba na birika ya shaba (brazen altar)

Hapa ndipo dhambi zilikuwa zinashughulikiwa.

Kwa hiyo, tunaona Mungu yuko mbinguni anamtuma Musa

Jangwani Mungu anakuwa na katika wingu na nguzo

Hema inapojengwa Mungu anashuka ardhini na waisrael wanajenga hema zao kumzunguka

Miili ya Wakristo ni maskani iliyozunguka Mungu na Mungu amezunguka. Mungu ndani yako nao ndani ya Mungu

Kwenye behewa ndipo wanyama walipochinjwa, ni eneo lilijaa damu kwa sababu hapa wanadamu na wanyama waliingia katika behewa

Wanyama walilipa bili za dhambi za mwaka mzima za wanadamu, Madeni ya aibu

Malipo yalilipwa kwa kutumia wanyama wasio na dhambi

Wanyama walitolewa uhai wao badala ya mwenye dhambi kutolewa uhai wake kwa sababu mshahara wa dhambi ni mauti
Unaona?

Ukombozi siku zote ni tukio la mbadilishano

Mungu alimwambia Adamu siku utakayokula tunda hilo utakufa, Kwa hiyo Mungu anapokuja bustanini ilikuwa amuue Adam au atafute uhai mbadala

Utakuwa unasema Adamu hakutakiwa kuuawana Mungu kwa sababu alikuwa amekufa tayari, ndio

Lakini Dhambi ya Adamu ilikuwa na vifo vitatu

1. Kifo cha kiroho cha mtenda dhambi
2. Kifo cha kimwili cha Adamu
3. Kifo cha fidia (sasa nazungumzia fidia)

Mungu alitafuta mnyama ili afe badala ya Adamu

Ili Adamu awe hai ilibidi mnyama afe, Hii ni picha ya Golgotha

Katika Mwanzo kabla ya sheria ya Musa makuhani walikuwa mababa na kazi yao ilikuwa ni kutoa sadaka kwa ajili ya dhambi za familia zao

Kwa hiyo kama sio baba huwezi kutoa sadaka

Kama sio kuhani huwezi kutoa sadaka

Hivyo, hapa Mungu anatoa sadaka ya kwa ajili ya dhambi kwa ajili ya adam

Hivyo kuhani wa kwanza ni Mungu

Mnyama ni picha ya Kristo kufa msalabani ili sisi tuioshi

Dhambi zangu ndizo zilizomuumiza msalabani. Hakufa msalabani kama Kristo bali kama……

Alikufa kama…..

Alikufa kwa niaba yangu ili niishi kwa niaba yake

Discuss: Wagalatia 2:20

Ndio maana Yesu alisema unapoomba “ombeni lolote kwa jina langu”

Unapoenda kwa Baba usitaje jina lako, usivae nguo zako hawezi kukuona wala kukusikia

Isaya 59:1-3

Kwa hiyo Mungu anapoangalia msalabani aliniona mimi na Yesu hakuwa msalabani ila mimi nili kuwa msalabani

Yesu=mimi
Mimi=Yesu

Kwa kuchubiliwa kwake mliponywa

Tukawa wazima sisi ni Yesu

Tulibadilishana. Tumebadilishana

Kinaleta wokovu muamala unafanyika madhabahuni

Unatupa dhambi zako madhabahuni

Tulimtupia dhambi zetu naye alitutupia haki

Nifuatilie vizuri utajua mengi

Hayo yote yanafanyika behewani sasa tuingie ndani, Patakatifu

Nataka uangale jambo muhimu kabla hajaenda mbali

1. Kadri unasogea kwa Mungu ndivyo kundi linapungua
2. Kila mtu aliweza kukusanyika nje lakini wachache waliweza kuingia behewani
3. Lakini ili uingie Patakatifu ulitakiwa kuwa kuhani

ìPitieni milango ya hekalu lake kwa shukrani, ingieni katika nyua zake kwa sifa. Mshukuruni na kulisifu jina lakeî Zaburi 100:4
Kila mtu anaweza kusifu, Kila mtu anaweza kumshukuru Mungu

Si ndiyo?

Zaburi 150 YAHWEH

Lakini linapokuwa suala la kuabudu, Makuhani wanaweza kuabudu.

Unaweza ukawa mwimbaji ukaimba nyimbo nzuri lakini linapokuja suala la kupewa siri za Mungu ukawa giza

Mungu anaposema nasi tunamjua

Yohana 4:24

Biblia haisemi wasifuo halisi, waimbao halisi bali waabuduo halisi

Kuabudu ni zaidi ya Kusifu, ni zaidi ya kushukuru

Kadri unavyokaribia kwa Mungu kwa kuabudu ndivyo ukaribu wa kuongea naye unazidi

Nyimbo: nyimbo za sifa zinakuweka karibu na watu

Nyimbo za kuabudu zinakuweka karibu na Mungu

Unaimba wimbo wa kuabudi unapoingia patakatifu lakini unaimba wimbo wa sifa unapoenda kwenye behewa

Unaposhukuru: Asante Mungu kwa kunipa watoto
Kwa kunipa mke
Kwa kunipa pikipiki
Kwa kunipa nyumba

Unapoabudu unamrudishia Mungu heshima!

Kusifu ni juu ya matendo ya Mungu

Kuabudu ni juu ya Mungu alivyo

Mika 6

Sasa karibu Patakatifu, ndani ya hema kama wewe ni kuhani kweli.

Mwambie jirani yako tunaingia Patakatifu

Unatakiwa kuwa kuhani ili uingie Patakatifu

 

1Petro 2:9-11
Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu; ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.
Mwambie jirani yako tuingie

Unapoingia unaachana na nuru ya jua hicho ndio kitu cha kwanza

Unaingia kwenye nuru ya mafunuo, tumeacha mionzi ya jua sasa tunaingia ndani kwa sababu ukifunikwa unapewa mambo matatu
1. Nguvu
2. Ulinzi
3. Mahitaji

Makuhani lilikuwa ni kundi lililochaguliwa iliwaweze kuingia patakatifu kwa niaba ya watu. Hii ndio nguvu ya Mungu kwa wanadamu

Kuhani anapoingia ndani alikuwa anamwakilisha Mwanadamu na Kuhani alipotoka kuwaendea watu alikuwa anamwakilisha Mungu.

Ngoja nikwambie nguvu walizokuwa nazo makuhani

Kama Askari wa Rumi wangemsulubisha Yesu bila
1. Kayafa kuhani kukubaliana kifo cha Yesu ingekuwa ni Mateso, ingekuwa ni kusulibiwa asingekuwa dhabihu
2. Yesu kuwa kuhani ingekuwa ni mateso tu

Kama unateswa na kuhani mkuu hakubaliana mateso unayopata utakuwa unapata taabu tu

Kama unateswa na sio kuhani, unapata taabu tu

1Petro 4:14

Kayafa ndiye anaibadili kifo cha Yesu kuwa dhabihu. Kwa sababu kuhani mkuu ndiye aliyekuwa na uwezo kumfanya mnyama awe dhabihu

Yesu asingekuwa Dhabihu kama kuhani asingehusika. Hili ni jambo la kwanza

Pili, Yesu ni kuhani aisye wa ukoo wa Kayafa, hivyo maovu waliyokusudia yalikuwa mema kwetu

Kwa kutumia vigezo vya kidunia, tunamwona Kayafa kwenye kifo cha Yesu kuwa dhabihu

Kwenye vigezo vya kimbingu tunaona Yesu ni kuwa dhabihu

Ndiyo, ni mtoa sadaka na sadaka, ni mtoa dhabihu na ni dhabihu yenyewe

 

Hakuna achukuaye uhai wangu bali nautoa uhai wangu kisha nitautwaa

Kama hivyo kama kuhani vipi wewe?

Warumi 12

1Yohana 3:16

Tunapoingia ndani ya hema tunakutana na mahitaji yetu

Sala ya Bwana:

Hema ni mahali tunapopate mkate wetu, chakula chetu. Mkate haupatikani nje.
Ni mahal pa mkate. Mahitaji yetu ndio muhimu sana

Mahitaji ya wokovu wetu!

Meza ya mkate wa wonyesho huonyesha mambo mawili:

1. Mahitaji ya kiroho

Mungu ni Yehiva yire- Mbuzi wa kafara, Kondoo wa kuuawa

Mbadala wa dhambi zetu

Alilipa gharama ya dhambi ili tukae hapa tulipokaaa

Alilipa ili haki isituhukumu

Alinyangíanywa nguo ili tuvae nguo-Kondoo alichunwa ili Adamu avae ngozi

2. Mahitaji ya kimwil

2Wakor. 9:7-10
Mathayo 6:28-33

Tunapoingia kwenye hema tunaenda kwenye mkate, Mkate wa minguni

Damu tumenawa kwenye birika (labor), Nimezaliwa! Nimeoshwa hatia na aibu ya dhambi

Nimepita mahali pa mauaji, kila wakati wanyama walipoingina kwenye Ua wan je, walijua hawatarudi

Ua wan je ni mahali pa hukumu, mahali pa kuchinja.

Ni eneo la damu. Harufu ya damu kila mahali, ni mahali pa uzazi. Sasa tunatoka mahali hapo

Waebrania 6:1-3

Tatizo la kanisa, tatizo la watu wengi leo ni kukwamba kwenye ua. Wanakwamba wakiwa wanagombaniana mafundiso, wengine wamekwama kwenye ubatizo

Kubishania siku ya kuabudu, kubishania kama umeokoka ama la

Umeingia kwenye mkate au uko kwenye ua wa nje? Huko ndio kuna mafundisho ya mabatizo na na changizo, na mafungu ya kumi

Umefungwa kwenye ua wan je?

Huu ni wakati wa kuondoka kwenye hiyo hatua

Unahangaika na dhambi kwa sababu haijalipwa kisawasawa? Kama bado unazungumzia mambo ya Ubatizo, kutawadha bado uko kwenye behewa

Soma tena Ufunuo: 11

Waebrania 10:19

Bado una hofu na watu. Bado unaogo pa yaliyokupata kambini, Bado uko nje behewani

Ilitakiwa yawe yameishia kwenye madhabahu ya shaba, ilitakiwa uwe unaoshwa kwenye birika

Sababu inakufanya uwe hivyo ulivyo ni vile hujalipa vya kutosha, vile hujanawa kisawasawa

Tunahitaji kwenda kwenye ukamilifu

Soma tena Waebrania 6
1Basi, tuyaache nyuma yale mafundisho ya mwanzomwanzo juu ya Kristo, tusonge mbele kwa yale yaliyokomaa, na sio kuendelea kuweka msingi kuhusu kuachana na matendo ya kifo, na juu ya kumwamini Mungu; 2mafundisho juu ya ubatizo na kuwekewa mikono; ufufuo wa wafu na hukumu ya milele.

Mwambilie jirani yako tuondoke, tuingie ndani.

Waebrania 6 inatuhimiza kuondoka na mkwamo wa mambo ya awali na kusonga mbele kwenye ukamilifu. Tusipofanya hivyo tunamsulubisha mwana Adamu mara ya pili na kumdhalilisha wazi wazi

Mwandishi anawaandikia Wayahudi walioanza kumwamini Yesu na kisha wakaanza kuona mashaka, wakaanza kuhitaji mafundisho ya awali

Ni muhimu ukaelewa hili, ni muhimu uijue Biblia yako

Tunatakiwa kuondoka kwenye Neema, twende kwenye utukufu, tunavuka viwango, tunaingina viwango vipya vya ukuaji

Kuna vitu vingi Patakatifu lakini naanza na meza ya mikate

Nataka nihakikishe unapata kila kitu

Madhabahu ya uani na birika vyote vilitengenezwa kwa shaba.

Tunapoingia ndani vitu vyote ni vya dhahabu
Weka akili kwamba tunatoka kwenye shaba tunaingia kwenye dhahabu

Tunatoka kuwa shaba tunaingia kuwa dhahabu

Dhahabu ni madinin yanayotunza hali yake hata ikiunguzwa. Thamani yake inazidi thamani ya shaba siku zote

Kama Waebrania isemavyo, tunapoingia ndani tunaend akwenye mambo bora. Unapozungumzia dhahabu, unazungumzia madini yaliyopita kwenye moto na kuwa mbele za Mungu

Kama ilikuwa dhahabu ilipoingia kwenye moto itakuwa dhahabu inapotoka kwenye moto

Kama ulikuwa umeokoka unapoingia kwenye majaribu utatoka ukiwa umeokoka unatoka kwenye jaribu

Kama ulikuwa Roho Mtakatifu unapoingia, utakuwa na Roho Mtakatfu unapotoka

Bwana anajua mapito yangu, Baada ya kunijaribu nitatoka!

Lakini yeye aijua njia niendeayo; Akisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu Ayubu 23:10

Nitatoka kama dhahabu. Jambo pekee utakalonifanyia ni kuunguza takataka na vumbi, huwezi kuunguza dhahabu

Hivyo ndivyo unavyotakiwa kusema unapokuwa unashambuliwa

Usipojua hali yako ulipoingina hutaijua hali yako unapotoka

MEZA YA MIKATE YA WONYESHO AU MEZA YA UKUMBUSHO

Kabla sijazungumzia mikate, Roho wa Mungu anaisukuma nizungumzie meza

Mikate lazima ikae mezani na Meza lazima iandaliwe

Unapokuwa na jaa kali na unafika nyumbani unakimblia mezani

Ndio maana watoto hawajui kwamba meza lazima iandaliwe

Meza ya mikate ya wonyesho ilitengenezwa kwa mbao za mshita

Kut. 25:23ìUtatengeneza meza ya mbao za mjohoro yenye urefu wa sentimita 88, upana sentimita 44 na kimo sentimita 66. 24Hiyo meza utaipaka dhahabu safi na kuizungushia utepe wa dhahabu.

Haikuwa meza kubwa kwasababu ilikuwa inabebwa wanahama

Mikate ilikuwa inatembea

Mti wa mshita unapatikana maeneo makame jangwani, ni imara.

Meza ilitengenezwa kwa mti unaopatikana jangwani na kupakwa dhahabu

Tunaanza kufika sehemu nzuri sasa

Niseme hili?

Mbao ya mshita-Waisraeli
Dhahabu-Mungu
Mbao ya Mshita ñWanadamu
Dhahabu-Mungu

Tunaingia kwenye agano lenyewe

Mungu anafanya uhusiano kati mti wa mshita na dhahabu. Kama ubao ungeungua ungeisha

Ubao ukiwa umepakwa dhahabu ukiuunguza hautaungua kwa sababu dhahabu imefunika

Iharibikayo inaoanishwa na isiyoharibika

Dhahabu inawakilisha Mungu na mbao inawakilisha mwanadamu

Kwa hiyo meza ilitokana na Mungu na wanadamu na ilikuwa inahama na watu

Meza ile ni mwili wa Yesu
Yohana 1:14

14Naye Neno akawa mwanadamu, akakaa kwetu. Nasi tumeuona utukufu wake, utukufu wake yeye aliye Mwana wa pekee wa Baba; amejaa neema na ukweli.

Yesu alichukua mwili (mbao) wakati yeye ni Mungu (dhahabu)

Wafil. 2:6

Oh, Mungu wangu, kumbe na msalaba ulikuwa ni mti uliobeba mti. Msalaba ni ubao uliobeba ubao

Kumbe msalaba anaosema Yesu niubebe inawezekana ni tofauti na ninavyofahamu

Mkate ulikuwa unahama jangwani

Makuhani walikuwa wanabeba meza ya mikate ya wonyesho

Ilikuwa ni lazima Yesu awe ubao. Yeye kuwa mbao ndiko kulikomfanya awe ndugu yangu. Ndiko kulikomfanya awe mwana Adamu

Ilikuwa ni lazima avae mwili wa kuahribika ili aguswe na hisia za madhaifu yangu

Kama meza ingetengenezwa kwa dhahabu tupu asingeweza kunisaidia katika kuomba kwangu

Warumi 8:26

Ali awe mwokozi wa ndugu zake aliutwa hali ya utumwa na Mungu alitengeneza meza kwa kutumia mti ili atuokoe kwa kutumia mti.

Kwa hiyo, Mwanadamu amewakilishwa na mti wa mshita, na Mungu amewakilishwa na dhahabu

Katika mtazamo wa agano jipya
Kwenye meza ile unamwona Yesu akiwa mti wa mshita na anakuwa dhahabu ili awe Imanueli Mathayo 1:21

Hiyo ni meza ya mikate ya wonyesho!

Oh Mungu wangu nihurumieÖ jambo hili ni zito!

Yesu anapozaliwa alizaliwa Behlehemu

ìnyumba ya mikateî

Mikate haikutakiwa kutolewa mezanix3

Mikate 12 (3×4)

Kuna kitu kipya nimepata, nje Waisraeli wameizunguka hema kambi 12 ndani ya hema kuna mikate 12 mezani nayo ilikuwa mzunguko

Wakati wa chakula cha mwisho kabla hajateswa aliketi chakulani yeye na mitume 12

Yesu ndiye mkate (chakula) wa kweli

Yohana 6:48

Waisrael walitembea jangwani na huku makuhani wanabeba vifaa vya hema

Miaka 40 nguo hazikuchakaa wala viatu havikuwaishia

Najiuliza pea za viatu ulizo nazo nyumbani

Idadi ya pea si muhimu, muhimu ni je safari inaendelea?

Tangu uzaliwe umevaa pea ngapi?

Inawezekana unaonekana husongi mbele lakini cha muhimu hurudi nyuma

Inawezekana inaoneka hujatoka lakini najua hujazama
Mungu hatakuacha jangwani, ataweka mlango wa kutokea

Huyo ndiye Mungu!

Alikuokoa ajali ilipotaka kkutoa uhai

Ajali zingine zinategenezwa na mapepo, kumbuka mawimbi ya baharini

Mawimbi hayataki uvuke lakini Mungu ameweka mlango wa kutokea

Sifanani na kule nilikotoka, ningekuonyesha nilokotoka wengine wangezimia

Ungeona kuzimu nilikoibuka ungenihurumia

Mwambie rafiki yako, bado nipo.

Kansa haijaniua

Njaa haijaniua

Lukemia haijaniua

Kisukari cha mapepo hakijaniua

Wachawi hawajaniua, bado nipo!

Una watu waliokuacha? Ambao walidhani bila wao utakwama?

Wapigie leo wambie bado nipo

Jipige picha watumie waambie bado nipo

Inawezekana uko jangwani lakini Mungu amekupa uziia japo uko jangwani

Kila ni k ifikiria wema wa Yesu na maumivu aliyopata, Napata nguvu ya kumaliza jangwa langu

Hata kama unapita katika jangwa gumu kiasi gani leo kuna mkate waliokula Waisraeli

MAANDALIZI YA MKATE
Mikate ya wonyesho haikuandaliwa na Mungu lakini ilitegenezwa kuwa kufuaata maelekezo ya Mungu

Meza ya Bwana inaandaliwa na wanadamu lakini kwa kufuata maelekezo ya Mungu

Kwa hiyo utengenezwaji wa mkate ni matokeo ya jitihada ya pamoja kati ya Mungu na mwanadamu

Mungu alitoa viungo, mwanadamu alitengeneza mkate

Lazima ujue kwamba unga wa mkate haukununuliwa tu dukani
Mkate ulitengenezwa kwa ngano iliyosagwa kwa mawe yaani ngano ambayo haijakobolewa

Unga wa dona ya ngano. Haukutakiwa kuwa unga wa keki ambao ni laini. Unga huu Mungu anauita unga safi

Mikate ilikuwa 12.

Mhh,, mikate inawakilisha watu

Kwa hiyo watu ni mkate na Yesu ni mkate

Unataka cheo wakati hutaki kuwa mkate. Mkate uliotokana na unga ulioburuzwa na mawe

Hujawahi kuwa mkate kwa sababu unataka cheo

Hakuna taji bila mijeredi

Unakuwa mkate baada kuburuzwa na mawe

Mathayo 26:26

Mungu anataka kukufanya mkate anakumega, anakuvunja kiburi, anavunja ubishi na ukaidi

Anakubadili kuwa majivu

Ndio, anakunyenyekeza

Kukufanya useme Amen kwa ajili ya mapenzi yake

Kuna wengine wanapitia magumu maishani kuliko unayofikiria, huo ndio wakati Mungu anakusaga uwe unga wa mkate

Unapitia magumu hadi unga wako una chumvi kwa machozi uliyotoa, mkate wakati mwingine unahitaji chumvi ili usioze

Umepitia upweke, na ukiwa na maumivu. Bwana amekuleta hapa leo

Ili ujue mkate

Kwa hiyo, mikate 12 ilipokuwa juu ya meza ilikuwa ni watu wa Israeli wakiwa mbele za Bwana usiku na mchana .

Kinachonipa furaha ni kwamba sio tu Mungu alijiweka kama mkate bali pia wana waisrael walikuwa mbele za Mungu kama mkate na wote walikuwa mezani

Warumi 12:1

Jambo la kwanza ninalotaka ujue ni kwamba:
1. Uko mezani pa Bwana
Majaribu, na taabu zote ulizopata zimekuwezesha kuwa chakula cha Bwana

Haijalishi unaomba kiasi gani maombi hayabadilishi mchakato wa Mungu juu yako.

Hakuna wakati meza ilibaki bila mikate

Mkate ulikaa wiki nzima na kubadilishwa siku ya sabato wakati wa kufukiza uvumba

Kumbuka uvumba ni maombi ni sala za watakatifu

 

Na makuhani walikula ile mikate wakati inabadilishwa. Hata wakati hema haitembei mikate ilikuwa mezani

Namwomba Mungu siku zote meza yangu isiishiwe mkate

Watu wasije kanisani na kukosa mkate

Nyumbani mwa Bwana kuwe na mkate kila siku mezani pake

Mezani kwangu kusikosekane mkate

Ukiwa kanisani ujue kutofautisha mchuzi na chakula, makelele na chakula cha Bwana

Kanisa limepoteza utambuzi, chakula kinatupwa wanakula mchuzi

Chakula halisi hukutia nguvu

Badala ya kuwa na uchungu, kisirani, na maumivu, Mungu amekuleta ili uutoe uhai wako mezani pake kama naye alivyoutoa uhai wake mezani ili uelewe kwamba michubuko inakupa Baraka

 

Yohana 3:16
1Yohana 3:16

Michubuko inakuimarisha

Michubuko inamfanya msichana kuwa mwanamke, Michubuko inamfanya mvulana kuwa mwanamume

Huwi mwanamume kwa sababu umesherehea birthday nyingi

Unakuwa mwanamume kwa sababu umeenda kuzimu na kusimama dhidi yake

Wewe ni mkate wa Mungu kama dhabihu iliyo hai

Ee Mungu nisaidie nitoke hapa,

Upande mmoja una mkate umetolewa kwa Mungu na upande wa pili ni Mungu anatupa mkate

Kwa sababu anasema hataiacha meza yangu bila chakula

Yesu ndiye Emmanuel, Atakuwa nawe Wakati wengine wameondoka

Atakuonyesha njia

Atakuwa nawe kwenye mawimbi

Atakuwa nawe jangwani

Atakuwa nawe watoto wako wakiondoka

Atakuwa nawe marafiki wakiondoka

Mana inashuka kutoka mbinguni, Mungu anawalisha watu wake

Mkate wa mbinguni

Mungu hukaa kati yetu nay eye ndiye maskani yetu, na sisi ni masikani yake

Ni mkate wa uzima

Kwa nini bado unataka vitunguu vya Misri? Yeye ndiye chakula cha mbinguni

Si unaona ulivyoshiba?

Neno halisi la Mungu ni chakula.

Neno halisi litavunja pingu

Shetani ni mjinga

Anamwambia Yesu ìgeuza mawe ya mkateî

Yesu anageuzaje mawe kuwa mkate wakati yeye ni mkate?

Usipojitambua utachanganya mkate na jiwe

Sifa na utukufu kwa Bwana!

Weka mkate mezani pa Bwana.

Weka mkate

In series Mahubiri