All Sermons
Bible Passage 1 Petro 2:10-12
This content is part of a series Mahubiri, in .

MATENDO YA KUHANI

Date preached October 19, 2025

GLOBAL CHURCH OF CHRIST JESUS TANZANIA
IDARA YA UMISHENI NA ELIMU

Limeandaliwa na Willy Emmanuel

KAZI ZA KUHANI

1 Petro 2:10-12
4Basi, mwendeeni Bwana! Yeye ndiye jiwe hai lililokataliwa na watu; lakini mbele ya Mungu ni jiwe teule na la thamani kubwa. 5Mwendeeni yeye kama mawe hai mkajengeke na kuwa nyumba ya kiroho ambamo mtatumikia kama makuhani watakatifu, kutolea tambiko za kiroho zenye kumpendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.

9Lakini nyinyi ni ukoo mteule, makuhani wa Mfalme, taifa takatifu; watu wake Mungu mwenyewe, mlioteuliwa kutangaza matendo makuu ya Mungu aliyewaiteni kutoka gizani, akawaingizeni katika mwanga wake mkuu. 10Wakati mmoja nyinyi hamkuwa watu wa Mungu, lakini sasa nyinyi ni watu wake; wakati mmoja hamkupewa huruma ya Mungu, lakini sasa mmepokea huruma.

Asante fundi aliyenikataa! Asante kwa kazi ambayo sikufanikiwa kuipata

Asante kwa wote walionifukuza!

Ukimwamini Mungu hutatahayarika

Rudi soma mstari wa 8,9

Somo letu ni Majukumu ya Makuhani, Mungu anataka ujue kwamba wewe ni kuhani

Hii haikufanya kuwana dharau kwa wahubiri, wazee wa kanisa kwa kujiona sawa na wao

Waebrania 13:7,17

Neno kuhani leo linapotumika wengi wanalitumia kumaanisha wahubiri
Wakumbukeni viongozi wenu waliowatangazieni neno la Mungu. Fikirini juu ya mwenendo wao, mkaige imani yao.

17Watiini viongozi wenu na kushika amri zao; wao huchunga roho zenu usiku na mchana, na watatoa ripoti ya utumishi wao mbele ya Mungu. Kama mkiwatii watafanya kazi zao kwa furaha, la sivyo, watazifanya kwa huzuni, na hiyo haitakuwa na faida kwenu.

Aya yetu inasema ìukuhani wa kifalmeî na Ukuhani mtakatifu

Wewe sio kuhani bali wewe ni ukuhani. Ni ofisi, wewe ni kazi yenyewe.

Tatizo ni pale tunaposhindwa kuuheshimu ukuhani.

Nirahisi kumsema kuhani mwenzio bila kujua unajisema na unaisema ofisi nzima

Unamvua nguo mwanaume mwenzio unajivua hata wewe

Kuhani kazi yake ni kumwakilisha Mungu anapokuwa na watu na kuwakilisha watu anapokuwa mbele za Mungu
Unamwakilisha nani unapokuwa mbele za Mungu?

Watoto wetu siku hizi wanaacha kanisa kwa sababu hawajafundishwa kutumika

Wamefundishwa maslahi u
Wamefundishwa kupokea, mara cha kupokea kinapoisha wanaondoka hata kama unawaona

Watoto siku hizi hawaoshi vyombo na unashangaa kwa nini mke wako anachoka

Huwafundishi

Lakini Biblia inasema sisi ni ìukuhani mtakatifuî. Sio kundi la waumini, sio tu kanisa, sio tu makuhani lakini ukuhani wa kifalme, Ukuhani mtakatifu

Tuna kazi tuliyoitiwa ambayo ni kutumika kama walivyotumika makuhani

Ukichunguza hema na hekalu, hakukuwa na kiti kwa ajili ya makuhani

Hakukuwa na pa kukalia

Hii kawaida ya kutokaa ni picha ya Mung mwenyewe. Sifa zilitakiwa kukwea mbele za Mungu daima,

Moshi wa sadaka ulitakiwa kufuka muda wote

Na bado tunaishi katika zama ambazo kazi tunayofanya ni kukaa

Na sababu huwezi kutumika ukiwa umekaa

MUNGU KUHANI WA KWANZA
Mwanzo 3:15

Biblia inasema Adam na Eva walisikia sauti ya Mungu bustanini

Sauti ya Mungu ndio neno la Mungu

Neno la Mungu ni Yesu

Ni lazima uelewe kwamba Mungu aliacha kupumzika na kuinuka ili amtumikie mwanadamu aliyeshindwa kumstumikia

Alishuka ili amtumikie mtumishi wake

Na anaposhuka alishuka kama kuhani

Alimjia Adamu kwa sababu alishindwa kwenda kwake

Tuna Mungu anakuja kwako unaposhindwa kwenda kwake

Si Adamu aliyemtafuta Mungu bali Mungu alimtafuta Adam

Hapa tunaona ukuhani mtakatifu kwa mara ya kwanza

Mungu akafanya ngozi ya mnyama na kumfunika mwanadamu

Damu inamwagika na mnyama anakufa

Muda wote Mungu anapomchinja mnyama, anachuna ngozi Adamu alisimama tu kwenye dhambi

Kwa sababu hawezi kumsaidia Mungu kumwokoa

Mungu ni kuahani wa kwanza tunayemwona katika Mwanzo na ni kuhani wa mwisho milele na milele

Unajiuliza kwa namna gani?

Yohana 3:16 Mungu alimtoa mwanawe wa pekee
Yohana 1:39 Yesu ni mwanakondoo wa Mungu

Hivyo Mungu ni kuhani alimtoa mwanakondoo kuwa dhabihu

Katika Agano la kale wanyama waliokuwa wanachinjwa walikuwa nembo ya Yesu na hivyo Yesu alichinjwa katika agano la kale na kwa hakika alichinjwa kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu

Mungu ndiye mwanzo na mwisho

Yesu ni kuhani pia kwa sababu ni mwana wa Mungu aliye kuhani. Kwa jinsi ya dunia

Mungu hajakuokoa kwa sababu una degree,

Hajakuokoa kwa sababu ni mzuri

Sio kwa sababu unaimba

Sio kwa sababu unahubiri vizuri

Alikuokoa kwa sababu yeye ni mtakatifu

Amekufanya uwe mteule

Kuna watu ni wazuri, lakin alichagua wewe! Alikusitiri

Umefika leo sio kwa sababu huna dhambi, bali kwa sababu amekustiri

MABABA NI MAKUHANI WA PILI
Kutoka kwa Mungu ukuhani ukwaangukia wanadamu

Sura ya nne tunamwona Habili na Kaini wakitoa sadaka

Habili anauawa kwa sababu ya majukumu yake ya kikuhani

Mathayo 23:35Hivyo lawama yote itawapateni kwa ajili ya damu yote ya watu wema iliyomwagwa juu ya ardhi. Naam, tangu kumwagwa damu ya Abeli ambaye hakuwa na hatia, mpaka ile ya Zakaria, mwana wa Barakia, ambaye mlimuua hekaluni kati ya patakatifu na madhabahu.

Sio tu Kaini alimuua Habili bali shetani alikuwa anajaribu kuua ukuhani
Kwa sababu ukuhani unawapatanisha wanadamu na Mungu

Alipomuua Habili damu iliendelea kulia

Alikufa lakini bado alikuwa ni kuhani. Moyo wake ualiacha kupumua lakini damu ilikuwa inaongea

Habili aliishi kama kuhani, alikufa akiwa kuhani Waebrania 12:24; 11:4.

Kwa nini Kaini alimuua Habili? Kwa sababu alikuwa kuhani, hakuiba, hakusema uongo, hakulewa bali sadaka zake zilipokelewa

Kwa nini Yesu aliuawa, alikuwa ni kuhani

Watu wanakuchukia kwa sababu unampenda Mungu,

Wanakuchukua kwa sababu unafuata ukweli wote

Mungu amekuokoa na wanakuchukia kwa sababu hujajiua

Waebrania 13:15

Sababu ya shetani kukuchukia hivi ni kwa sababu ameshindwa kukunyangíanya sifa mdomoni mwako. Yeye alikuwa malaika wa sifa, sauti yake ilikuwa nzuri

Hapendi uwe na sauti nzuri ya kumwimbia Mungu

Anataka uimbe kivivu

Alipoanguka, nafasi ilikuwa wazi, Mungu amekupa nafasi yake umwimbie sifa na huimbi?

ìNa tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, tunda la midomo yetuî

Sifa ni dhabihu

Miili yetu ni dhabihu

Yesu ni dhabihu

Kwanini usiwe kuhani?

Ni lazima uimbe hadi shetani akuchukie

Mdomoni mwako mnatoka maji ya uzima lakin kuna mauti.

Kinywani mwako kuna uzima kwa ajili ya watu wa Mungu lakini mauti kwa ajili ya mapepo na shetani

Unatoa sifa, unatoa dhabihu ya sifa unatoa mauti kwa shetani lakini unakuwa faraja, unakuwa maonyo, unakuwa nguvu kwa watu wa Mungu

Zaburi 66:1
1Enyi watu wote duniani mshangilieni Mungu!
2Imbeni juu ya utukufu wa jina lake,
mtoleeni sifa tukufu!
3Mwambieni Mungu: ìMatendo yako ni ya ajabu mno!
Nguvu zako ni kubwa mno hata maadui zako wanajikunyata kwa hofu.
4Dunia yote inakuabudu;
watu wote wanakuimbia sifa!î

Tunapoimba tunatoa sadaka

Tunapoimba tunaunguza dhabihu

Tupoimba tunatekeleza majukumu ya ukuhani

Malaki 2

8ìBali nyinyi makuhani mmegeuka mkaiacha njia ya haki. Mafundisho yenu yamewaongoza watu wengi katika kutenda mabaya. Mmelivunja agano nililofanya nanyi. 9Nami pia nitawafanya mdharauliwe na kupuuzwa na Waisraeli, kwa sababu hamkuzifuata njia zangu, na mnapowafundisha watu wangu mnapendelea baadhi yao.î

Soma na Malaki 1:13

Sema na mwenzio ìwewe ni kuhaniî Sadaka zako za sifa ni nzima?

Kama unahubiri unatoa sadaka kwa Mungu

Turudi kwenye eneo la somo letu

Ukuhani wa mababa

Mababa walikuwa makuhani

Nuhu alikuwa kuhani

Ile kuwa mtoto wa Nuhu au kuwa mke au mkwe wa Nuhu ilitosha kabisa kuwa salama

Umekuwa chini ya mbawa za kuhani

Hawakutakiwa kutoa chochote

Hawakutakiwa kubatizwa

Lakini kuwa familia ya Nuhu ilitosha kuwaokoa na gharika
Jiulize, unahusiana na nani? Uhusiano wako unaweza kukuokoa au kukupoteza

Unaendaga Kanisani jumapili tu?

Sio tu Nuhu alijenga safina kwa ajili ya familia yake lakini pia alijenga madhabahu kwa ajili ya shukrani

Unajua kwa nini baadhi ya watu ni vigumu kwao kujenga Kanisa? Unajua kwanini ni vigumu kujenga madhabahu?

Kwa sababu hawajui kama ni makuhani hata kama wana hela

Ukiwa kuhani utagharamia lakini pia haitakuwa vigumu kumwambia Mungu akubariki

Unashindwa kufanya hivyo kwa sababu ya ujuaji wako

Unasema sio lazima, ni hiari, kwa kadri ya kufanikiwa

Kwa kadri unavyoendelea kuwa mjuaji ndivyo kiburi kinavyotafuna Baraka zako na suala la kutoa linaenda mbali

Ndio maana mambo mengi yamekwama, umekuwa mpokeaji tu.

Unavunja sheria ya mbegu na mavuno. Kupanda na kuvuna

Hata kama huiamini biblia yako basi liamini neno la Mungu

Amini sheria asili ya mbegu

Kama kila siku unapokea na hujui kutoa, jifunze kwenye kupumua unakuwa hai kama unatoa pumuzi na hutoi utaugua, utakufa

Ulemavu wa kitabia

Ibrahimu alikuwa Kuhani

MWanzo 22

ìkule kuabuduî

Kwetu sisi ukisema naenda kuabudu tunarajia kukuona ukiwa umebeba Biblia ambayo huiamini

Umebeba tenzi ambayo huimbi

Sio lazima ubebe matoleo kama chenji za maandazi hazijabakia

Ukifika kanisani unasinzia- Kuhani anasinzia

Katika familia ya kuhani wakisema tunaenda kuabudu kitu cha kwanza kuja akili ilikuwa ni matoleo
Ni sadaka

Kabla hawafika mahali pa Ibada Isaka alimuuliza baba yake

Kuni zipo, kisu kipo lakini Sadaka siioni

Hii inaonyesha kwamba haikuwa mara ya kwanza

Hii inaonyesha kwamba kwenye nyumba ya Ibrahimu kulikuwana kawaida ya ibada, Kiasi cha Isaka kujua kinachokosekana

Watoto wengi hawaoni kinachokosekana

Hawakuoni unapoomba sebuleni, hawakuoni unasoma Neno la Mungu

Mara nyingi wanakuona unasoma Biblia

Ibrahimu alimchinja mnyama akaita ibada

Kama haombi mtoto ataombaje?

Haya yaliwezekana kwa sababu Ibrahimu alikuwa kuhani

Namna pekee ya kumfundisha mwanao kutoa ni wewe kujitoa kwa Mungu

Hiyo ndio nguvu ya baba aliye kuhani

Ibrahimu alitoa sadaka mbele ya Isaka na Isaka aliona

Ukuhani wa Ibrahimu uliwezesha Isaka kujua kinachokosekana

Anayefuata ni Melkisedeki:

Mwanzo 14:18Naye Melkisedeki, mfalme wa mji wa Salemu, ambaye alikuwa kuhani wa Mungu Mkuu, akaleta mkate na divai, 19akambariki Abramu akisema,
ìAbramu na abarikiwe na Mungu Mkuu,
Muumba mbingu na dunia!
20Na atukuzwe Mungu Mkuu,
aliyewatia adui zako mikononi mwako!î
Naye Abramu akampa Melkisedeki mchango wake sehemu ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo.

Zaburi 110:4 Mwenyezi-Mungu amekuapia wala hatabadili nia yake:
ìWewe ni kuhani milele kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.î

Waebrania 5:6-11; 6:6- 7;

1Huyo Melkisedeki alikuwa mfalme wa Salemu, na kuhani wa Mungu Mkuu. Abrahamu alipokuwa anarudi kutoka vitani ambako aliwaua wafalme, Melkisedeki alikutana naye, akambariki, 2naye Abrahamu akampa sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo. (Maana ya kwanza ya jina Melkisedeki ni ìMfalme wa Uadilifu;î na, kwa vile yeye alikuwa mfalme wa Salemu, jina lake pia lina maana ya ìMfalme wa Amani.î

Kwa mara ya kwanza tunamsoma akiwa mfalme wa Salem na kuhani wa Salemu

Sasa tazama Kuhani Ibrahimu anakutana na kuhani Melkisedeki

Kwa nini Ibrahimu alitoa fungu la kumi kwa Melkisedeki wakati naye ni kuhani?

Ni swali ambao wajuzi wa Biblia wamejaribu kujibu bila mafanikio

Leo nataka ujue Neno la Mungu kwa ajili ya swali hili.

Ibrahimu alikuwa ni kuhani lakini hakuwa mfalme

Kwa hiyo alikuwa anatoa huduma za ukuhani wakati Melkisedeki alikuwa anafanya ukuhani wa ukuhani

Ukuhani na ufalme unapokutana ndipo ukuhani wa kifalme unatokea

Biblia inasema Yesu ni mfalme mfano wa Melkisedeki, ni kuhani kama melikisedeki

Biblia inasema sisi ni makuhani wa kifalme.

Kuhani wa kifalme anayefanana na Yesu ambaye anafananishwa na Wakristo ni Melkisedeki

Alitoa Mkate na Divai

Yesu usiku aliotolewa alitoa Mkate na Divai kwa sababu alikuwa anauanzisha ukuhani wa kifalme

Ndio maana tunashiriki meza ya Bwana. Kukuhani wa kifalme hutoa divai na makate

Alichokifanya Melkisedeki katika Mwanzo wa Agano la kale, Yesu alifanya mwanzo wa Agano jipya akiwa Yerusalemu usiku aliosalitiwa

Mungu anataka ufahamu kwamba wewe ni kuhani na ni mfalme

Hivyo tembea kama mfalme-mtawala Mwanzo 1:27-28
Tembea kama kuhani-Mtumishi wa Mungu na watu

Ukuhani wa kifalme

Unaitwa Melkisedeki

Mtu mwema anajua jinsi ya mfalme na jinsi ya kuwa kuhani

Tatizo tulilo nalo leo ni kwamba tunaona kama tunatakiwa kuchagua

Katika Kutoka 3:1; 18:5,12
YETHRO

Hapo Yethro, baba mkwe wa Mose, akamtolea Mungu sadaka za kuteketezwa na tambiko. Naye Aroni akaja pamoja na wazee wa Israeli ili kula chakula pamoja na Yethro, mbele ya Mwenyezi-Mungu.

Musa alijifunza kuwa mfalme akiwa Misri lakin ili kuwa kuhani alijifunza kwa Yethro

Kuna mambo utajifunza kwa farao na mengine utajifunza kwa Yethro

Inachukuwa watu kumwandaa kuhani ambaye ni mfalme

Musa hakuogopa kwenda ikilu kumwambia Farao Mungu anataka uwaachie watu wake kwa sababu anajua ikulu ilivyo

Musa alijua kwenda kwa farao kwa sababu alifundishwa na Farao na alijua kuwaokoa watu kwa sabau amefundishwa na Yethro

Mungu anapokuita kutumika kama kuhani atakutuma kwa Yethro.

Unamjua Yethro?

Wengi wetu tumefundishwa na Farao lakini hatukubahatika kufundishwa na Yethro ndio maana hatuna unyenyekevu, hatuna kushuka, hatujui kuwa mtumishi ni kuwa mdogo

Alichokufundisha Farao kitakufanya ujue kutawala na sio kutumikia

Jihadhari na watu waliosoma kwa Farao

Ukuhani wa kifalme: Mungu anasema Wakristo ni ukuhani wa kifalme na sio kuhani wa kifalme bali ukuhani wa kifalme

Nakuhitaji uwe imara kama mfalme lakini nakuhitaji uwe mnyenyekevu ili unisaidie kutumika unapotakiwa kutumika

Nakuhitaji uwe kiongozi na mtumishi

UKUHANI WA WALAWI
Kuna tofauti ndogo kati ya kuitwa kwa haruni na kuitwa watoto wake

Hata kama alikuwa na watoto 4 lakini alipata upaka upako moja

Harufu ya watoto inafanana ya baba

Anachosema baba kinabaki na wewe
Mwanzo 49

Wakati waisraeli wako Sinai Lawi alikuwa ameshakufa

Simioni na lawi walilaaniwa

Musa alipokuwa mlimani, Haruni alitengeneza sanamu na watu wakaabudu wakiwa uchi.

Mungu akawaua wote ambao waliabudu isipokuwa waliochagua upande wa Mungu

Nataka uone kwa nini Mungu aliwaua

Walitengeneza sanamu iliyofanana na miungu ya Misri

Mungu aliwatoa Misri lakini Misri haikutoka ndani yao

Mungu hakushindwa kuwaingiza Kanaani bali wao walishindwa kuondoa mikate ya Misri ndani yao

Umeuacha ulimwengu lakini ulimwengu haujakuacha

Misri imetoka ndani yako?

Naweza kujua kwa jinsi unavyowatendea wengine

Naweza kujua kwa namna unavyovaa

Naweza kujua kwa jinsi unavyoongea

Kwa jinsi unavyotukana wengine

Na ugomvi ulionao

Unaweza kuwa shemansi na bado ukawa unagombania mipaka ya mashamba

Kama unataka kuondoka Misri acha kuabudu sanamu za Misri

Walawi walisema sisi tutakuwa upande wa Bwana, tamko hilo lilimfanya awape urithi kwenye nyumba ya Mungu

Walawi walichukua msimamo wakati wengine wanasitasita

Nataka nikuulize leo

Uko upande gani?

Uko upande gani?

Ili Mungu akufanye kuwa kuhani lazima ujibu swali hili leo

Kazi imebaki kwako

Leo jione umekutana na ukuhani

Leo jione umekutana na ufalme

Leo jione kuwa taifa la Mungu

Kabla hujasema lolote, kabla hujafunua kinywa chako

Tambua uwezo wa uzima na mauti uko kwenye ulimi wako

Kuna nguvu kubwa kwenye ulimi wako kiasi cha kuua huduma ya mwingine

Kwa sababu umekuwa kuhani, kwa sababu umewekwa wakfu

Anasema

Basi, acheni uovu wote;

Huruhusiwi kuishi na visirani, chuki

uongo, unafiki, wivu na maneno ya kashfa visiweko tena

ìya kila namnaî

Huwezi kuona Uovu wote,

Huwezi kuona hula, Huwezi kuuona unafiki, huwezi kuuona wivu na masingizio

Mambo haya yapo kanisani lakini kanisa linahubiri mambo yanyoonekana

Kama una dhambi isiyoonekana uko huru kumsema mwenye dhambi inayoonekana

Kwa hiyo unaweza kusingizia na hakuna atakayekemea

Unaweza kuanza majungu nab ado ukawa unanena kwa lugha

Unaweza kuwa na wivu, unaweza kuwa mnafiki na unaweza kuna hila

Kwa sababu unaruhusiwa na dhambi isiyoonekana

Unaweza ukawa na hila alimradi hatukuoni ukiwa unazini

Kwa kadri ambavyo hatuiioni dhambi endelea kuifanya

Lakini nataka ujue kwamba kama unataka kuwa kuhani, Ili kuingia patakatifu ni lazima unawe kwenye birika

Mwanakondoo alichinjwa mahali ambapo pana madhabahu na birika
Madhabahu uliunguza kabisa ile sadaka ya dhambi na makuhani hawakuruhusiwa kuingia Patakatifu bila kunawa

Kwenye madhabahu kuna matendo ya dhambi, kwenye birika tuna tabia ya dhambi

Ni kwenye birika ndipo kuhani alitakiwa kukubali kwamba mikono yake ni michafu

Ndicho alichomaanisha Pilato aliponawa mikono

Katika Ezekiel 33 Nisipokuonya damu yako itakuwa mikononi mwangu

Kwa hiyo makuhani ambao walikuwa watumishi wa Mungu walipaswa kunawa

Hakuna mwenye haki

Kwa sababu wewe ni kuhani Mungu anasema ameguswa na chuki uliyonayo

Ameguswa na kisirani chako

Ameguswa na hila yako

Ameguswa na uongo wako

Chukua matendo yako ukawnawe

Sio kwamba umesema uongo, bali kwa sababu umejiepusha kuwa mkweli

Kuna mtu anaumizwa lakini unaujua ukweli husemi

Hiyo ndio hila

Umeacha watu wanaamini uzushi kwa sababu ya hila yakok

UNAFIKI: Umekuwa ukiwasema watoto wa wengine mpaka lilipokukuta na watoto wako. Sasa unataka kanisa liombe kwa ajili ya watoto wako

Wivu: Hapo ndipo tunapokutana na wenye chuki, unawakosa watu walikokuzidi wala hutaki kuwapongeza

Hizi ni dhambi zisizoonekana

Dhambi hizi zinaweza kuishi na wewe bila kutoka mdomoni

Ewe kuhani,

Mungu anasema wekeni mbali;

Kama kuna Baraka nitakayopata mwaka huu, natakiwa ninawe wmili na roho
2Wakor.7:1Basi, wapenzi wangu, tukiwa tumepewa ahadi hizi zote, na tujitakase na chochote kiwezacho kuchafua miili na roho zetu, tuwe watakatifu kabisa na kuishi kwa kumcha Mungu.

Kumbuka Waisrael walitangatanga jangwani mpaka wakafa kwa sababu ya mdomo

Walinungíunika na kulalamika kwamba heri wangefia Misri

Mungu akawapa mikate wakasema mana

Kila wakati Mungu anapotaka kukubariki anakutana na mdomo wako

Akimbariki mwingine unaanza mdomo

Unamsingizia, unamlaani, unamsengenya

Acha mdomo ubarikiwe

Sijui kama neno linakusaidia kama ulizoea kusaidiwa na Biblia?

MaandikoÖ

Wewe ni ukuhani wa kifalme!

Acha kuongea kihuni!

Umekuwa katika madhabahu ya shaba, Umempa Yesu maisha yako,

Amekusamehe kunyongwa kwako

Lakini mdomo wako uko kama Wamisri

Wakati mwingine sio mapepo yanazuia kubarikiwa bali na tabia zako ni kizuizi

Sio kwasababu hujaweka maisha yako kwenye madhabahu bali ni kwasababu hujasahau mabaya uliyotendewa na watu

Na unadhani kutosamehe kunamuumiza aliyekukosea lakini kutosamehe kunachelewesha Baraka zako

Mungu anavunjika moyo kila anapouona moyo wako

Leo ameniambia nikwambie

Yaache yote madhabahuni, piga hatua hadi kwenye birika ukanawe kisha ingia Patakatifu

Ameniambia nikwambie wewe ni ukuhani wa kifalme

Mungu anavunjika moyo anaoona hila

Anapoona hasira

Anapoona uongo

Kama kuna lolote ndani yako limekufanya uwe na uchungu hivi

Limekufanya usilale usiku
Linakufanya uwachukie watu Fulani

Linakufanya uumie kwa sababu wengine wamepewa cheo ambacho ulikitaka

Ni adui ameichachusha roho yako

Roho yako ina maambukizi

Mungu atakusafisha leo

Simama niombe na wewe

Mafuta ya Mungu yakufunike, yakutakase

Mafuta ya Mungu yakutie kimvuri
Mafuta ya Mungu yakuokoe

Wewe ni uzao mteule, ukuhani wa kifalme

 

In series Mahubiri