All Sermons
Bible Passage Marko 5:2-28
This content is part of a series Mahubiri, in .

USIONDOKE KAMA ULIVYOKUJA

Date preached October 5, 2025

GLOBAL CHURCH OF CHRIST JESUS TANZANIA
IDARA YA UMISHENI NA ELIMU

Limeandaliwa na Willy Emmanuel

USIONDOKE KAMA ULIVYOKUJA
Marko 5:2-28

1. Kufungwa
2. Makubalini
3. Kulia
4. Kumkimbilia Yesu

UTANGULIZI

Pamoja na kwamba sio mji wa wayahudi na pamoja na dhoruba bado alidhamiria kwenda

Tuko katika dunia ambayo watu wa kanisani wanaenda waliko watu wa kanisani.

Katika sura iliyotangulia tunaona lililotokea na katika surah ii tunaona kwa nini ilitokea

* Sura hii inatuambia kwa nini kulitokea mawimbi baharini.
* Sura hii inatunambia kwa nini Yesu alingíangíania kwenda ambako atafukuzwa

Nikijua utanifukuza siwezi hata kukusalilmia

Yesu anaenda ambako hakuna ìamenî

Anaenda kwa makusudi na sio kwa ajili ya kundi bali kwa ajili ya mtu mmoja
Leo tuko juu juu kwa ajili ya kujali umati kubwa na tunapuuza mtu

Nimejifunza kwamba ukipenda watu utavutia umati

Lakini huwezi kuvuta umati kama hupendi watu kwa sababu upendo ni sumaku na inavuta tunaowapenda

Alipofika, alikutana na mtu aliyeishi makaburini. Hakuwa mzimu, hakuwa maiti bali mtu mwenye mapepo aliyekuwa anaishi makaburini

Mapepo yalimsihi sana Yesu ayaruhusu yawaingine nguruwe

Ndio maana tunajua hii haikuwa nchi ya Wayahudi maana Wayahudi hawafugi nguruwe badala yake wanafuga kondoo

Hayo ndio mazungmzo ya Yesu na mapepo. Mazungumzo ya mema na mabaya. Haya ni mazungumzo ambayo lazima uwe rohoni ndio unaweza kufanya mawasiliano na kusikia. Yesu kama roho anaziamuru roho chafu

Yesu anapokutana na mwenye mapepo mapepo huondoka.

Alipoyaruhusu kuwaingia nguruwe na mapepo yalipowaingia nguruwe nguruwe walitumbukia baharini, bahari ambayo Yesu amenusurika kuzama yakazama yenyewe na nguruwe

Sasa unaanza kuelewa kwa nini bahari ilitaka kumzamisha Yesu

Wanaotaka kukuzamisha watazama wenyewe! Tena watakuomba wasione mafanikio yako, watazama huku unawaangalia

Maji huwakilisa uhai kwa mwanadamu lakini ni kaburi kwa nguvu za giza

Dunia ilizaliwa kutoka kwenye maji
Watoto wanazaliwa kutoka kwenye maji
Wakati waovu wanazamishwa safina iliokoa nane kwenye maji
Waisraeli waliokoka kwa maji wakati Farao anazama kwenye maji
Kabla ya kuingia patakatifu kulikuwa na birika ya maji
Naamani aliambiwa akajichovye kwenye maji ya Yordani
Mtu hazaliwi kiroho bila maji na roho
Maji ni kaburi kwa sababu tunapobatizwa kwenye maji tunazikwa, tunauzika utu wa shetani
Mungu husafiha kanisa kwa neno katika maji
Mbele ya kiti cha enzi kuna bahari ya kioo
Pepop amtokapo mtu hupitia sehemu ambayo haina maji siku hiyo waliingizwa kwenye maji! Unadhani nini kilitokea

Kama unaona Yesu anayaruhusu mapepo yaingie kwenye nguruwe sasa unajua kwa nini

Nguruwe walikuwa 2,000 na mapepo yalikuwa ni jeshi (lejion) kikosi cha askari kuanzia 3,000-6,000. Kama mapepo yote yaliwaingia nguruwe 2,000 ina maana kila nguruwe aliingiwa na mapepo matatu.

Kama uliona Yule mtu akikata pingu na minyororo ni kwa sababu alikuwa na jeshi.

Sasa unajua kwa nini

Wachungaji wa nguruwe walikimbia- siwalaumu

Wanyeji walipokuja na kumkuta aliyekuwa na amepona na ametulia ni kama anasema ìhey habari gani?î

Akiwa amevaa nguo na akili timamu. Kufunguliwa kwake kuliwatisha

Hivi unajua kwamba wanaofurahia mateso yako ni wale wanaokufunga

Kufunguliwa kwako kunawatisha sana, Shetani anatishika, Kuzimu inatetemeka

Kanisa limefungwa mno kiufahamu, ukijaribu kulifungua kanisa kuna watu wanatishika

Hakuna aliyefurahia kufunguliwa kwake

Watu wanakuwa na amani ukiendelea kufungwa, ni kufunguliwa ndiko kunakowatisha

Mapepo yalimsihi Yesu, naoo wanamsihi Yesu aondoke. Hicho ndicho walichofanya! Walimfukuza Yesu badala kumsihi akae nao

Kwanini?

Nawaza kwanini pia?

Kwanini nguruwe walikuwa wanalishwa makaburini ambako analala mwenye mapepo?

Umejua kwa nini walimfukuza Yesu?

Ngoja niendelee, kwanini Yesu aliyakubalia mapepo yawaingine nguruwe? Kwanini awe tayari kusababisha hasara? Utajua kwanini utakapojua kwa nini Farao anapofuata vyombo walivyoazima waisraeli alizamishwa

Kuna watu wananufaika na kuugua kwako
Kuna ndugu wanakuvuruga ili wachume utajiri
Kuna watu wananufaika unapodhalilika
Familia yako haieleweki lakini kuna watu wananufaika

Unajiuliza kwanini, ndio maana Yesu alimwambia aende nyumbani kwao kwa ndugu zake! Akwahubirie alitendewa

Kwani kwao kulikuwa ni wapi, ni kule walikotoka waliomfukuza Yesu au ni kwingine? Ili ujue hili jiulize kwa nini alitaka kwenda na Yesu na sio kwenda kwao

Kama Yesu alimfungua mwenye mapepo 6,000 atashindwa kukufungua?
Mwambie uliyekuja naye, ìusiondoke kama ulivyokuja.

Mwisho wa Utangulizi:

Baba Mungu katika Jina la Yesu, Litakase neno hili katika mioyo ya watu wako
Nakushukuru kwa yale uliyptuandalia, pita katikati yetu Bwana.Naamini utatufungua,naamini utatukomboa, naamini utatuponya

Utaturejesha, Utatufanya upya na hatutaondoka kama tulivyokuja

Katika Jina La Yesu!

Amen.
Wanadamu ni nafsi tatu na hali hiyo inatufanya tuwe katika hali isiyotabirika

Sisi ni roho, sisi sio mwili.

Sisi ni roho tuna nafsi yenye akili, kumbukumbu na hisia na tunaishi kwenye mwili

Sisi ni roho, tuna nafsi, tunaishi kwenye mwili lakini hatuihi mwilini

Ndio maana Paulo anasema nyumba iliyo ya maskani hii ikiharibika nina jingo lingine

Kwa maneni mengine, kifo hakiondoi uhai kifo kinahamisha uhai kwenda kwenye jingo lingine

Mimi sio mwili ila naishi kwenye mwili. Utu wangu wa nje (mwili) unaponyauka kama majani ya mtini utu wangu wa ndani unafanywa upya

Unaweza kupima typhoid kkumbe tatizo liko rohoni ila linaonekana mwilini.
Unaweza kuwa na kitu kinachohambulia utu wako wa ndani lakini lakini dalili zikaonekana mwilini

Ayah ii inashughulika na yote matatu na nataka ujue kwamba jambo moja huathiri lingine

Umewahi kujiuliza kwanini kuna wakati unashindwa kupata usingizi?

Unachukua dawa za usingizi. Dawa za usingizi zimetengenezwa kwa ajili ya mwili na tatizo lako liko kichwani

Tatizo tunalolisoma hapa ni kwamba walikuwa wanajaribu kulidhibiti tatizo la kiroho kwa kutumia kamba za kimwili.

Tatizo lake lilikuwa linaumiza mwili wake pia

2Na alipokwisha kushuka katika mashua, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu;

Unafungaje pingu roho?
Walikuwa wanatibu dalili na sio chanzo.

Najiuliza kama tunatibu dalili au chanzo cha Kanisa kurudi nyuma?

Je tunafanya maombi ili tuwe nafuu kwa nje wakati chanzo kipo ndani/

Mfano; watu wanene mara nyingi wanaugua kisukari kwa hiyo wanaepuka baadhi ya vyakula, lakini inawezekana sicho unachokula bali kinachokutafuna ndicho kinachokufanya uwe mnene. Kwa hiyo ukitibu inarudi tena

Huu ni wakati wa kwenda ndani ya dalili na kushuhgulikia chanzo.

Ili unielewe vizuri na upate ujumbe wako kwenye aya hii ni kwamba ni lazima ukubali kwamba inawezekana unayemchukia unamchukia kimakosa.

Kwa sababu unaangalia tu alichofanya sio kwa nini alifanya alichofanya na unaweza ukawafanya wasiwe vile unavyotamani kwa nini unaendelea kufanyia kama wakosaji

Maudhui ya aya hii ni WANNE WANAONDOSHWA

Najaribu kuchimba aya hii

1. Walimwondosha mwenye mapepo kutoka kijijini
2. Yesu aliyaondosha mapepo
3. Yesu alimwondosha makaburini aliyekuwa na mapepo
4. Wenyeji walimwondosha Yesu kutoka kwao, kutoka makaburini

Heri Yesu akuondoshe leo kutoka mabaurini, ukahubiri

Mathayo 28:18-20

Kuna watu bila kujali na bila kukusikiliza watakufukuza kwenye maisha yao.

Watakutenga kwa sababu wako kwenye nafasi ambayo hakuna anayeweza kuwatenga

Angeshuka Mungu kufanya tathimini kati yenu wao ndio wangetengwa.

Mungu anataka kukuondosha kutoka makaburini ambako ndugu zako na rafiki zako walikuacha ufie huko

Tunapoisoma aya tunaona mtu mwenye ndugu na marafiki ni mkiwa, ni wa mitaani kwa sababu baadaye tunaona Yesu anamwambia aende nyumbani kwa jamaa zake

Jamaa zake ni ndugu zake au rafiki zake

Kama una marafiki unawezaje kuishia makaburini. Hapa mwenye ndugu anaishi makaburini

Ukweli ni kwamba, hata marafiki wanachoka!

Hata ndugu wanachoka

Kuna marafiki waliochoka hapa?

Kuna ndugu waliochoka hapa?

Jihadhari usichoshe marafiki

Jiepushe usichoshendugu

Kila siku wewe tu wewe tu, matatizo yako kla siku unawamabia watu wala hakuna siku unawambia neno la Baraka!

Hata upendo unachoka! Hata watoaji na wafadhili wanachoka. Usiruhusu mtu azidishe kukusaidia, kitakachotokea watachoka na kukuacha makaburini

Yule mtu anaishi makaburini ambako tunawaacha tunaowapenda

Japokuwa hajafa bado, walimwacha makaburini, sio tu aliachwa makaburini bali na upendo wao kwa Yule mtu ulikuwa umekufa uliachwa makaburini

Walimwacha kule ajifie, ila alikuwa hajafa. Kama unaniacha makaburini huku umenifunga kwa pingu na minyororo unataka nife

Laiti wasingemfunga ili angalau ajitafutie chakula

Lakini ukinitupa kaburini huku umenifunga unasubiri nife halafu unashangaa nikizikata pingu na minyororo-nataka niishi

Unashanga kwanini unanikuta milimani ñSitaki kufia makaburini

Siwezi kufanana na yanayonizunguka kwenyemaisha yangu-nitakata pingu na minyororo yao.

Nitaenda milimani nitafakari kwa maumivu kwa nini niliowathamini kama ndugu wamenitupa

Kwanini niliowathamini kama rafiki wameniacha makaburini nife peke yangu

Naumia, sioni thamani yangu duniani, najichukia, najichoma, najikata

Bora nife kwa kujikata mwenyewe na mawe kuliko kufia makaburini

Jambo moja ninalojua ni kwamba wanavyochukulia walivyonitupa makaburini ni tofauti na ninavyojichukulia

Sijafa bado!

Ukiishi na walio kaburini sio muda unakuwa kama wao.
Waambie sijafa bado!
Kuna watu wanasubiri upige magoti ili wapate ulicho nacho

Kuna watu wanasubiri ufe na wameshaanza kuchagua mashamba watakayorithi, wengine wamechangua ngíombe watakayochukua, wangine wamejichagulia mali zako

Kuna watu wanajiandaa kuoa mke wako ukifa

Wengine wamejiandaa kuolewa na mume wako

Wengi wap ni ndug uzako!

Wengi ni rafiki zako!

Waambie sijafa bado

Inawezekana nateseka, inawezekana niko kwenye matatizo lakini sijafa kiroho bado!

Nataka nimwabie Shetani leo, sijafa

Bado kuna muujiza unakuja kwa ajili ya maisha yangu!

Kwa ajili ya familia yangu!

Kwa ajili ya huduma yangu!

Inawezekana naugua

Inawezekana nimechanganyikiwa,

Lakini jambo moja unalotakiwa kulizingatia ni kwamba sijafa!

Makaburini ni mahali pa kumbukumbu

Ni mahali pa maombolezo

Na ndicho hasa kilichomfanya alien a kuomboleza kwa sababu aliwekwa mahali pa kumbukumbu na maombolezo

Makaburini ni mahali tunapotembelea lakini hatuishi makaburini na Yesu anakuja kumwokoa

Yesu amekuja leo kukuokoa usiishi kwenye mambo yaliyokufa, usiishi miongoni mwa waliokufa!

Ufunuo 3:8
Waebrania 9:14
Mambo tuliyoyazika, mambo tuliyopoteza, na shughuli ambazo hazikufanikiwa
Ni kawaida kukumbuka mambo ya nyuma inasaida kupata hekima ya maisha yajayo lakini ni jambo moja kukumbuka mabaya ya nyuma na jambo lingine kuchua mto na kwenda kulala kwenye mambo ya nyuma

Kuna watu hapa waishi kwenye makaburi ya hasara walizopata

Makaburi ya makosa yao na matatizo yao

Unapoanza kuishi makaburini ni ishara tosha ya kwa nini umepoa umekuwa vuguvugu na sio muda unakuwa baridi

Unajua kuwa kuna watu wanakwambia mambo uliyofanya miaka 20-30 iliyopita. Umevuka huko na bado wanahisi uko vilevile, wanaishi kwenye makaburi.

Ndio maana malaika alimwambia Mariamu usimtafute Yesu miongoni waliokufa
Luka 24:13

Kwa sababu ukikaa na makaburi kwa muda wa kutosha unakuwa kama rafiki zako

Yesu alitembelea kaburini lakini hakuishi kaburini anaishi mbinguni!

Waambie msinitafute makaburini, inawezekana nilikuwa makaburini uliponiona lakin unitarajie mimi kuishi makaburini

Ulikutana na mimi ijumaa, lakini leo sio ijumaa!

Nimefufuka na nguvu zote!

Naongea na wewe ulizimia,

Naongea na wewe uliyeanguka

Wewe uliyezimima kwa sababu ya vita ulizopigwa, umesinginziwa, umewekewa mitego na njama zikunase!

Waliokuchukia, Waliokukimbia!

Waambie ilikuwa ijumaa!

Usiishi walipokuacha

Usiishi walipokutupa

Usiishi walipokuuacha adui zako!

Wakikuona, waambie mlikosea! Njama hazikufanikiwa! Siwezi kufia hapa!

Mliniacha hapa lakini sitafia hapa!

Nilitembelea makaburini sitaishi makuburini!

Nikwambie jambo zuri? Waliokuacha makaburini utawaacha makaburini

Wewe utachapa kazi ya Bwana!

Bwana atakutuma ukahubiri, Bwana hatabaki makaburini

Waambie, nitatoka makaburini kwa gharama yoyote! Iwe kwa maombi, iwe kwa kuimba,iwe kwa kwa kuhubiri, nitatoka hapa maana hapafanani na nyumbani

Waambie Yesu aliyemwambie Zakayo mkuyu haufanani na nyumbani atanirudisha nyumbani

Kwa sababu mahali wamekuacha hapafanani na hatima yako. Walikuahidi kukusomesha

Walikuahidi kukuajiri

Walikuahidi vingi ili ubaki makaburini maana ahadi zao ni pingu

Ahadi zao ni minyororo!

Sitafia uliponikuta, sitafia uliponiacha

Usinifunge na ahadi zako, Usinifunge na minyororo matendo yangu ya zamani wakati matendo yako ya zamani husimulii.

Natoka!
Naondoka!

Nakuacha wewe makaburini. Uombleze juu ya nguruwe wako!

Uomboleze juu ya mapepo mliyonifunga nayo!

Natoka!

Natoka kwenye madeni, natoka kwenye umasikini, hata kwa kukjivuta natoka hata kwa gharama ya kujichovya Yordani

Umekuwa mpweke muda mrefu, Umetengwa muda mrefu

Umpweke umekutesa na kukuumiza. Kataa kufungiwa kwenye kabati, kata kufungiwa kwenye mafundisho manyonge

Usifungiwe makaburini!

Najua mnafurahia mimi kuishi hivi nilivyo, najua hampendi nikiishi kwa furaha, lakin natoka

Ninatoka hata kama mnaendelea kunisema, Semeni yote mnayoweza lakin nataka

Najua hamtasema nitakapoishi kwenye ahadi za Mungu, nitakapoishi kwenye ndoto zangu
Nitapambania njia yangu, naogopa lakin nitatoka, inawezekana natetemeka lakini natoka

Chochote ulichonifunga nacho navunja!

Umefika kwenye kongamano ambalo Mungu anakuita uingie kwenye upana wa uhubiri wako

Mungu anakuinua juu ya pito linalokukandamiza na ni wakati wa kuvunja

MAKABURINI:

1. Walimtupa makaburini
2. Yesu aliyafukuza mapepo makaburini-makaburi ni mashimo
3. Wenye nguruwe walimfukuza Yesu atoke
4. Yesu alimtoa aliyekuwa mapepo atoke Kaburini arudi nyumbani
5. Kaburini walibaki waliomtupa, Makaburini walibaki waliomfukuza Yesu, Kaburini watabaki waliopanga njama za kukuzika!

III. MINYORORO NA PINGU:

Pingu na minyororo walizomfunga nazo zilikuwa kwa ajili ya kumbakisha walipotaka afie

Ndio! Vyeo vingine wanavyokupa ni pingu na minyororo

Maneno ya watu dhidi yako ni pingu

Ahadi zao kwako ni pingu!

Zawadi zao ni pingu, uendelee kuishi makaburini. Toka!

Walikusemea manuizi tangu ukiwa mtoto yamekuwa pingu. Vunja

Wanakufunga kwenye minyororo ya mitazamo yao

Vunja, vunja!

Roho Mtakatifu amenituma kwako, niivunje minyororo, nivunje pingu

Navunja pingu alizokufunga baba yako, alizokufunga mama yako, walizokufunga ndugu zako, walizokufunga rafiki zako, walizokufunga viongozi wako navunja!

Tusi alilokutukana mwalimu shuleni lilikuwa pingu mpaka uachukia hesabu, ukachukia shule, ukachukia sayansi.

Vunja!
Kuna watu wamekuja kwenye kongamano na wengine wamekuja kuvunja pingu na minyororo-usiondoke kama ulivyokuja!

Kuwa muhibiri haimaanishi kwamba huwezi kuwa na maendeleo

Ukila nyama wanasema ni hela za kanisa-vunja hizo pingu
Ukinunua pikipiki wanasema ni hela za kanisa

Ukianzisha misheni watakwambia misheni gani haina mzungu-vunja pingu hizo

Ndio maana niko hapa kukwambia hata muhubiri anaweza kula nyama choma!

Kila pingu ina lengo la kukufanya mnyonge, inalenga kukufanya mpole ili uishi kwenye vipimo vyao

Vunja pingu!

Biblia inasema hakuna aliyeweza kumfunga! Angalau huyu alikuwa nafuu kuliko wengi wetu.

Mwambie jirani yako ìhuwezi kunifungaî

Sengenya sana, lakini huwezi kunifunga

Tukana sana lakini huwezi kunifunga

IV. MADHARA YA MAJERAHA YA PINGU:

Je Yule mtu alikubaliana na kufungwa?

Hapana!

Angekubaliana na pingu, asingeweza kumkimbilia Yesu

Ukikubali pingu hutafunguliwa

Nataka nione Kongamano hili likikufungua chumbani kwako, sebuleni, jikoni, na nataka kuona ukifunguliwa kanisani.

Kwa hiyo tumeona makaburi hadi minyororo na kutoka kwenye minyororo hadi kulia

KULIA MCHANA NA USIKU
Kila unapoishi miongoni mwa waliokufa unazuiwa na minyoro ambapo wengine wanafurahi kuzuiwa kwako

Watu watakufunga kwa faida ya furaha. Unasema mimi ni mtulivu na mpole kwa sababu naishi kwenye vipimo vyako
Kufungwa kwake ilikuwa ni utulivu wa ndugu zake na rafiki zake

Kufunguliwa ilikuwa ni usumbufu kwa ndugu zake,

Nawaza kama alikuwa na mke na watoto

Nawaza kama alikwa na wazazi

Jiepushe na watu wanaojifanya wanakujua sana!

Sisemi Yule mtu hakuwa na matatizo, na sisemi alikuwa na matatizo ila nasema alikuwa pia na ahadi

Na unapokuwa umenaswa kati ya matatizo yako na ahadi watu wanakufunga na kukutupa makaburini

Lakini kila walipomfunga alivunja minyoyoro. Walifunga nje wakati tatizo liko ndani, walifunga mwili wakati tatizo liko rohoni, Waliufunga mwili wakati tatizo haliko kwenye mwili

Yatazame maisha yako yalivyaa alama za minyororo watu walizojaribu kukufunga

Yatazame maisha yako ya nyuma uone walichokusemea watu kwamba hutafika mbali
Utaishia hapohapo. Wote walikosea! Mungu amekufungua

Sio lazima unipende lakini huwezi kunifunga

Hakuna awezaye kumfunga aliyefunguliwa na Mungu mhh,

5Na sikuzote, usiku na mchana, alikuwako makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikatakata kwa mawe.

Nataka niseme na wewe kuhusu nyakati za kulia

Sijui ulivyolelewa, lakini mimi nililelewa katika mazingira kwamba huruhusiwi kulia.

Kulia kunauma! Lakini hata kama kunauma nilitamani kulia ili nipate nafuu ya maumivu.

Majonzi hayaondoki kama machozi hayatoki. Kulia ni muhimu

Kulia hakukufanyi uwe na nguvu,kunakufanya uishiwe nguvu

Kama hujanielewa ni hivi; Kuna wakati maishani mwako inabidi ulie hata kama hujafiwa.

Inawezekana unalia kwa ajili ya nguvu kubwa uliyumia kufanya kazi ambayo hakuna anayekujali

Unalia kwa ajili ya muda ulioutumia kusaidia watu ambao leo wanakufunga pingu

Unalia jinsi ambavyo unatamani watu wajue unachojua lakin hawataki

Kuna mambo mengi ya kulilia unapoomboleza

Mume wako analia lakini anangoja ulale ndio analia

Mke wako anangoja ulale ndio analia

Kama unataka Mungu asikie, Lia!

Mtu asipolia anaweza kujinyonga

Kuna kilio kinaweza kumfikia Mungu1 Kilio kinakamata Mungu!

Kama huamini muulize Bartimayo,

Kadri walivyomnyamazisha ndivyo alizidi kulia

Alilia hadi Yesu alisimama. Kuna kilio ambacho kinashika Bwana, anasimama!

Waulize Waisraeli
Kilio chako kitamfanya Mungu asikilize na kuona kinachoendelea

Nikujulishe?

Kilio kilimfanya Yesu adhamirie kuvuka ngíambo.

Kilio chake kilmfanya Yesu avumilie upinzani baharini

Daudi anasema maskini Amelia na Mungu amesikia kilio chake, na kumwokoa

Kama utafungua kinywana kulia, Mungu angekuokoa

Tatizo sio Mungu, tatizo ni kwamba mdomo wako umeufunga, ukifungua mdomo wako, Mungu atakuja kukuokoa

Sishangai kuona upepo haukuzuia Yesu, Sishangai kuona mawimbi hayakumzuia Yesu. Ilikuwa ni lazima avuke ngíambo maana kulikuwa na kilio

Fungua mdomo!

Fungua mdomo

Tema, lisema
Sijali likoje lakini tema

Yesu atasimama kama utalia. Kilio kinamfikia Mungu!

Najau huamini, lakini muulize Habili, Damu ilipolia Mungu alizungumza akasema nimesikia kilio cha damu!

Unataka kujua damu nini? Damu ni uhai na uhai ni pumzi, Lia!

Walipotupa Yona, Alilia na Mungu alisikia

Hana alilia!

Lia Mungu atasikia.

Biblia inasema alilia mpaka akaoenekana kama mlevi kumbe amelewa maumivu, kumbe amelewa maombi
Ndugu yangu acha kuguna, Lia

Biblia inasema Yesu alilia

Kama Yesu anaweza kulia kila mtu anaweza kulia

Katika kitabu cha ufunuo Biblia inasema, nikasikia kilio cha roho zilizo chini ya madhabahu zikisema hata liniÖ.

Sema hata lini? X3

Mwambie Mungu imetosha!

Hutafia makaburini, Usifumbe mdomo

Biblia inasema;
5Na sikuzote, usiku na mchana, alikuwako makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikatakata kwa mawe.

Alilia makaburini na milimani, Bila kujali uko juu au uko chini Lia. Unaelewa kwa nini wengine wanalia wakiwa bondeni lakini ogopa watu wanaolia wakiwa mlimani

Ukiwa mlimani hakuna anayetarajia kukuona unalia

Wamezoea kuona walio bondeni kulia

Wasomi wanalila, Wenye vyeo wanalia

Kulia ni zawadi kutoka kwa Mungu

Usipokitapika kilicho ndani yako kitakutafuna, kitakupa kichefuchefu, Kitakupa presha, kitakupa sukari na vidonda vya tumbo

Acha kuweka siri

Lia

Usirudi nyumbani na hali uliyo nayo
.

KWANINI YULE MTU ALIMKIMBILIA YESU?

Ni lazima nikwambie kwanini yule mtu alimkimbilia Yesu

Hata kama alimkmbilia Yesu, mapepo bado yalikuwa yanaendelea kuongea

Safari hii yaliongea na anayemkimbilia

Alikuwa anakimbia, mapepo yalikuwa yanaongea

mapepo yalikuwa yanaongea lakini hayakuweza kumzuia kumkimbilia Yesu

Unatakiwa umkimbilie Yesu hata kama Iblisi bado anaongea kihwani mwako!

Sijali amekwambia nini, Sijali amemwambia nini Yesu kwa ajili yako

Ninachojua ni kwamba natakiwa kukimbia hata kama anaongea

Kuna watu wanataka kukusaidia, lakini adui ameenda kuongea naye wasikusaidie

Kuna watu wanataka kukusomesha, lakini adui amewambia huna tabia nzuri

Usikate tamaa! mkimbilie Yesu hata kama anaongea na Yesu

Wengine wameomba kwa Mungu uporomoke kiuchumi, mkimbilie Mungu tu

Nataka uelewe hili kwa sababu ni muhimu sana

Tumeona Mawimbi baharini, tumeona mateso ya kuishi makaburini, tumeona pingu na minyororo ya ndugu na marafiki, Tumeona kilio hadi kujikata kata mwenyewe

Sasa nataka nizungumzie kujikatakata

Biblia inasema alikuwa najikatakata mwili wake mwenyewe

Kila kitu kilichotokea nyuma kilitokana na watu wengine

Walimfunga minyororo na pingu lakini alizikata-Kumbuka tumesema pingu ni manuizi, lawama, mashitaka na maneno ya maadui kwamba usiende popote

Walimtupa makaburini

Lakini alipokuwa peke yake, alijikatakata

Sasa nazama, nazama hapa kwenye kujikata

Nataka uyafahamu madhara uliyojifanyia mwenyewe, Mambo ulijiumiza mwenyewe baada ya kutupwa, baada ya kusahauliwa

Baada ya kukimbiwa! Baada ya kusalitiwa!

Tazama hili;

Huyu mtu yuko makaburini, ana marafiki ambao hawezi kuwafikia

Ana ndugu na wazazi ambao hawezi kuwafikia

Ana watu aliowahi kuwasaidia

Lakini yuko makaburini.

Ana maisha mambayo hawezi kuyafikia

Ana kitanda lakini hawezi kulalia,

Ana nyumba labda

Unapotoka kutendewa mabaya na watu ambao ilikuwa wakutendee mema kwa jinsi ulivyowajali,

Unapotoka kusemwa vibaya na watu ambao hata hawasemi ukweli,

Kwa kuwa huwezi kushindana nao, kinachofuata ni lazima ujifunze kushindana moyo wako ili ushinde.

Linalofuata unaanza kuchukia uliyotendewa badala ya kumchukia aliyekutendea

Hatua hiyo inakuingiza kwenye kujidhuru

Kila kitu na watu wanaokuzunguka kinapokugeuka

Hasira yake ilirudi ndani yake kumtafuna!

Hiyo inaitwa msongo wa mawazo

Msongo ni hasira iliyotumbukia ndani

Hasira usipoitoa nje inarudi ndani

Ikitumbukia ndani inakufanya ujikate mwenyewe

Itakufanya uwe adui yako mwenyewe!

Mungu nihurumie, najisikia kuhubiri..

Itakufanya ujiue,

Biblia inasema, wakati yuko peke yake alikuwa najikata mwili mzima

Kwa nini ajikate!

Inaitwa dawa ya maumizi-maumivu kwa maumivu

Umesalitiwa unajinyonga!

Umedhulumiwa unajua!

Kudhulumiwa ni maumivu na kujiua ni maumivu!

Maumivu kwa maumivu ni pale watu wanapojaribu kutibu maumimvu ya ndani kwa kujiumiza kwa nje

Wanaokutukana wanakuumiza kwa ndani, maumivu yao hayatoki damu lakini wewe unajiumiza kwa vidonda vya tumbo

Wanaokusaliti wanakuumiza kwa ndani lakini wewe unajinyonga

Ukweli ni kwamba kujikatakata hakukuondoa maumivu ya moyo.

Haijalishi unakata kimwili au kiakili unafanya hivyo ili kuepuka maumivu uliyo nayo

Unazima moto kwa kutumia moto

Hii ni tabia ya kujiua

Ungeweza kuitoa hasira kabla haijakimbilia ndani

Ungefanikiwa kimaisha lakini unajikata

Ungeheshimiwa lakini umejikata, unajiona huna faida

Umekataa kufanikiwa kwa sababu umekubali kujiumiza

Kila wakati ukionewa huli chakula, huendi shambani, unashinda umeinama. Unajikata

Unajiona huna maana, kwa sababu wamekuona huna maana

Kinamfanya adui akufanyie hivyo ni kwa sababu anataka ujiue mwenyewe bila yeye kukuua

Kataa kufa!

Kila wakati unapata nafasi ya kupanda juu lakini unajiona huna lolote

Lakini, mashua ilipofika ufukweni…..

Habari ilibadilika!

Mashua imefika leo, imekufikia

usiondoke kama ulivyokuja

Mashua ilipofika, alimkimbilia Yesu,

Mapepo 6000 yako ndani ya huyu mtu hayakumzuia kumkimbilia Yesu

Kama uko tayari kumkimbilia Yesu hakuna litakalokuzuia

Mapepo hayakuwa na uwezo wa kujificha tena, hivyo kabla hajaongea yaliongea yenyewe

7 akapiga kelele kwa sauti kuu, akasema, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakuapisha kwa Mungu usinitese. 8Kwa sababu amemwambia, Ewe pepo mchafu, mtoke mtu huyu. 9Akamwuliza, Jina lako nani? Akamjibu, Jina langu ni Legioni, kwa kuwa tu wengi. 10Akamsihi sana asiwapeleke nje ya nchi ile.

Mapepo yalijua Yesu ni roho na yenyewe ni roho

Yakobo 2:19

MAshetani yanaamini na kutetemeka

Kama huamini waulize wana wa Skewa.

MAPEPO YANA MIPAKA YA UTAWALA:

Mengine ni ya familia, mengine ni ya kijiji, mengine ni ya wilaya, mkoa Taifa, ukanda, Bara na dunia

Nakwenda kinyuma na mapepo ya mkoa wenu yanayotawala eneo la maisha yako

Kuna eneo lina nafsi shetani anataka kulikalia kwenye Kanisa-

Na hataki kuondoka kwenye hili eneo mpaka amalize muda wa malengo. Mpaka akuharibu kabisa, Mpaka akuue kabisa, Mpaka ufukiwe kaburini

Aliingina kwenye ukoo muda mrefu ndio maana sehemu hatari kukaa ni misibani!

Muda wangu hautoshi kukufundisha msiba na mapepo. Mapepop hayana mwili na yanahitaji mwili ili kufanya kazi yao

Hayawezi kufanya kazi hewani yanahitaji mwili wa kufanyia kazi

Na yakasema, kama unatutoa tunaomba tuwaingine nguruwe!

Inawezekana kulikuwana mabishano kabla ya kufikia uamuzi wa kuwaingina nguruwe

Unajiuliza najuaje, najua kwa sababu biblia ni ramani, sio nyumba ya kuishi. Yameandikwa tu yale ya kutufikisha tunakokwenda

Kwa hiyo Jeshi moja la mapepo lililokuwa kwa mtu mmoja,

Oh mtu mmoja!

ìKushindana kwetu si juu ya damu na nyama bali ni juu yaÖÖ.majeshi ya pepo wabayaî

Yule aliishi na jeshi la mapepo ambapo nguruwe 2000 hawakuweza kuishi nao hata kwa dakika moja

Nguruwe walipoingiwa na mapepo yaliyokuwa kwa mtu mmoja, nguruwe walijiua

Nguruwe waliojiua, mapepo yalikosa pa kukaa na yako kwenye maji

Kumbuka pepo amtokapo mtu hutafuta mahali pasipo na maji

Nguruwe walisema,
Nguruwe walisema, ni heri kuzama kwenye maji kuliko kuishi na mapepo

Nami nakwambia nakwambia ni heri kubatizwa kuliko kuishi na mapepo

Ndio maana ubatizo ni muhimu, kwa sababu sio tu unaondoa dhambi lakin pia unamzamisha shetani, unayazamisha mapepo

Ndio maana Yesu mpaka leo analisafisha kanisa kwa neno na kwa maji.
Kanisa, nimesema Kanisa.

Nguruwe wanaona ni heri kufa kuliko na hali ambayo kanisa linaishi nayo.

Umekuwa ukipambana na mambo ambayo ni magumu kiasi cha kukuua

Nayatangazia mapepo leo, mwili wako sio hekalu lao

Sijui utaenda wapi baada ya kutoka maburini lakini najua utakuondoka hapa tofauti na vile ulivyokuja

Simama mfukuze shetani mbele yako!

ì Wala msimpe shetani nafasiî

Jifunike na damu ya Yesu, Jifunike na ubatizo, kila napotaka kurudi akute sio wewe ni Yesu

ìwaliobatizwa katika Kristo wamemvaa Kristoî

Tangu sasa mtu asinitaabisheÖî

Yachanganye mapepo, yape msongo wa mawazo, yatoke yakidhani yatakuwa hai kmbe yanaenda kuangamia

Sio lazima moto uyaunguze, hata maji ni sumu yao

Hata maji ni kaburi lao.

Tumia siku ya leo kuachana nayo. Unalala nayo, unakula nayo yazamishe baharini

Swala si yanaenda wapi bali ni kwamba yalipo si mahali pao!

Mapepo yakatumbukia majiniÖ

JAMBO LA MWISHO:

Mapepo yanatafute mahali pasipo na maji, yazamishe kwenye maji

Aliyekuwa anajkatakata makaburini, Yesu alipomaliza tatizo lake, alirudiwa na fahamu zake

Ndugu zake hawakufurahi ndio hofu yake,

Hakujua mapepo yamezamishwa, ndio iliyokuwa hofu yake
Aliogopa kurudi nyumbani, nyumbani ndiko yalikomwanzia

ìNataka niende na weweî na anamwambia nina kazi na wewe huku Dekapoli

Kwa mwonekano wa nje kuna furaha lakini upande wa pili kuna hofu ya kurudi nyumbani

Jambo lililomzuia kwenda nyumbani lilikuwa ni kuwa nyumbani

Hahahaha, kuwa nyumbani kunatisha, kunaleta hofu

Nyumbani ndiko kunakupiga vita, nyumbani wanakuwana amani ukifeli.

Nyumbani. Yesu akamwambia rudi nyumbani.

Tukiwa kwa watu tunacheka, watu wanadhani tuna furaha lakini tunaogopa nyumbani.

Jambo gumu kwa mwanaume ni kurudi nyumbani

Hata kama akienda kimwiliÖwanagapi tuko nyumbani, wangapi tuko hapa!

Kwenda nyumbani ambako hujaenda nyumbani ndiko kunasababisha wanaume wengi wakifika wanazunguka nyumba kwanza, wanaenda chumbani ndippo wanakuja sebuleni kwa sababu wanaiona nyumba kama kazi mpya.

Yesu akamwambia nenda nyumbani ili uwe nyumbani, nyumbani ni kuzuri lakin ni gharama kuwa nyumbani

ìAdui za mtu ni wale wa nyumbani mwake mwenyeweî

Yesu alivumilia vita ya baharini kabla hajamkomboa Yule mtu na hakutaka aondoke naye.

Hata kama wamemkataa Yesu, hata kama wamemfukuza Yesu, Yesu anataka Yule mtu akawe mahubiri ya kila siku kwao

Akachukue nafasi iliyokaliwa

Hahitaji kuandika kitabu wala kuandika Biblia bali akae kibalazani akinywa chai

Ni mahubiri tosha

Amani yako ya ni kitisho tosha bila Yesu mwenyewe

Umekuwa ukiwaza kwa nini unapanda lakini huvuni kama ulivyopanda

Umekuwa unawaza kwanini unatoa lakini hufanikiwa

Ni kwa sababu Mungu amekuwa akipeleka Baraka nyumbani kwako lakini uko makaburini umebadilishana Baraka na makaburi

Ukiwa nyumbani, nyumbani hasa ambako hujikati unaiona thamani yako, huwazi kujiiua kwa kushindwa

Ubunifu wako unakuwa juu

Mafanikio yanaongezeka

Amani inapoongezeka, nguvu inaongezeka!

Vile unapojikuta ukilala hujui kama funguo za chumbani zitakuwepo ili utoke au mtagombana hadi ushindwe kutoka

Unapoona unawaza kurudi nyumbani lakin unatamani ukute wamelala na hujui kama watakufungulia-huwezi kuwa nguvu, leo rudi nyumbani ukahubiri mambo aliyokufanyia Yesu!

Mafanikio yako, amani yako, nguvu yako vinahitaji uwepo wako lakini umekuwa ukiishi makaburini

Mtu Yule alitaka kuodnoka na Yesu, hakujua kama Yesu ametangulia nyumbani na anamsubiri yeye

Unaporudi nyumbani, Yesu ametangulia. Unajiuliza kivipi.

ZAkayo aliambiwa wokovu umefika nyumbani mwake wakati yuko juu ya mti

Yesu alimwambia pepo akahubiri, ìnami niko pamoja nayi hata ukamilifu wa dahariî

Sio kwamba Mungu hakupendi ila wewe ndio hujipendi. Watu wasiojipenda hudhani hawapendi

Watu wasiojiamini huwawamini wengine

Wasiojipenda ndio wasiopenda na wasiojiamini ndio ambao hawawaamini wengine

Mungu anataka urudi nyumbani, ukae nyumbani na wewe mwenyewe

Acha kujumiza kwa ajili ya mambo ambayo huwezi kuyadilisha, rudi nyumbani. Yaliyotokea huwezi kuyabadilisha. Yaliyopita yako makaburini usiende kuishi kuishi makaburini.

Rudi nyumbani!

Acha kuishi na waliokufa

Makaburi tunayatembelea hatuishi, makaburi sio nyumbani. Hakuna hoteli makaburini

Jambo moja ninalijua kwa hakika ni kwamba hutaondoka kama ulivyokuja.

Utaondoka umenichukia
Utaondoka ukiwa umefukuza hahahaha
Kwa sababu nimekuzamisha majini ulipodhani utaishi kwenye nguruwe kwa muda ili umrudie tena aliyepona

Usiondoke kabla hujabadilika.

Kwa nini unawaza kujiumiza, Mungu anajua, Anajua

Ndio maana;

ìKwamaana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanawe pekee ili kilaÖî

Mungu anakuppenda na hakuna anayekupenda kama Mungu-Kafanye kazi yake

Hakuna anayeweza kuchukuliana na wewe kama Mungu

Ukiwa uchi usiogope, Mungu anakujua

Mungu akubariki, awabariki wanao na binti zako

Natamka kuongezeka kwako

Natangaza mafanikio katika maisha yako. Sio utajiri tu bali hekima na ujasiri na nguvu na kuridhika

Umetoka mbali

Kwa nini uendelee kuishi na uchungu na hasira

Lolote linalokutesa na kukupeleka makabirini achana nalo leo. Rudishamani yako

Acha kuhangaika kuweka viraka kwenye mioyo iliyokukimbia, mioyo iliyokutupa

Mioyo iliyokuchukia

Pata amani, keti kibalazani wakuone. Waambie sijafa

Usihangaike kubadilisha akili zao.

Mungu ameniambia nikwambie USIONDOKE KAMA ULIVYOKUJA!

Sasa nyosha mikono juu shetani ajue hujafa!

Tuombe.

 

In series Mahubiri