GLOBAL CHURCH OF CHRIST JESUS TANZANIA
IDARA YA UMISHENI NA ELIMU
Limeandaliwa na Willy Emmanuel
USIONDOKE NA UPEPO
Yohana 8:3-11
3Basi, waalimu wa sheria na Mafarisayo wakamletea mwanamke mmoja aliyefumaniwa katika uzinzi. Wakamsimamisha katikati yao. 4Kisha wakamwuliza Yesu, ìMwalimu! Mwanamke huyu alifumaniwa katika uzinzi. 5Katika sheria yetu Mose alituamuru mwanamke kama huyu apigwe mawe. Basi, wewe wasemaje?î 6Walisema hivyo kumjaribu, wapate kisa cha kumshtaki. Lakini Yesu akainama chini, akaandika ardhini kwa kidole. 7Walipozidi kumwuliza, Yesu akainuka, akawaambia, ìMtu asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza kumpiga jiwe.î 8Kisha akainama tena, akawa anaandika ardhini. 9Waliposikia hivyo, wakaanza kutoweka mmojammoja, wakitangulia wazee. Yesu akabaki peke yake, na yule mwanamke amesimama palepale. 10Yesu alipoinuka akamwuliza huyo mwanamke, ìWako wapi wale watu? Je, hakuna hata mmoja aliyekuhukumu?î 11Huyo mwanamke akamjibu, ìBwana, hakuna hata mmoja!î Naye Yesu akamwambia, ìWala mimi sikuhukumu. Nenda zako; na tangu sasa usitende dhambi tena
Katika mstari wa 3 tunaambiwa kwamba Waandishi na mafarisayo walimleta mwanamke ìaliyemfumaniwa kwenye uzinziî
Umati huu wa watu baadaye unasemwa kama ìwaoî
Mara nyingi ni ìwaoî ni kweli ni wao!
Huwezi kuwa na mvi bila kukabiliana na mapungufu
Ni heri kuongoza kanisa kuliko kuongoza viongozi
Kadri unavyozeeka inabidi uangalie nyuma.
Inashangaza tunavyowahukumu watu huku tukijitetea wenyewe
Kwenye Saikolojia kuna kitu kinaitwa ìakili ya mkumboî
Ni wakati watu wanapokasirika na watu wengine wanadakia tu na ukweli hauzungumzwi
Ukweli unakuwa lengo baya
Unaona kwenye mitandao ya kijamii, watu wana hasira wakati hata hawajui kwanini wana hasira
Wanapost na kutweet
Jambo linaenea wala hakuna anayefuatilia ukweli
Ni rahisi kudakia na kuwa sehemu ya kundi lenye hasira
Nayasema haya kwa sababu wengi mnadhani ni vigumu kupeperushwa na upepo
Kanisani kwenu kuna mikumbo
Kwenye ukoo kuna mikumbo na shuleni kuna mikumbo
Kama hujiungi na upepo wao wana namna ambayo tunaita ìkukutupia kimvuriî ambapo wanakuwekea wapelelezi wajue kwa nini hujaungana nao
Kwa sababu umekataa kuwa wao
Watakuadhibu kwa sababu tu umeamua ìkufikiriî na kuwa na ìakiliî yako mwenyewe
Wanakuadhibu kwa sababu ya kusubiri ukweli
Hii inatokana na ukweli kwamba wanadamu wanataka kuendana na walio karibu nao
Tunapenda kupenda kupendwa
Utasikia usiposema hivi wewe sio mwenzetu
Wewe sio kanisa letu
Wewe sio kanisa la kweli
Wewe sio familia yetu
Watakwambia hivyo hadi uwe wao
Malcolm Gladwell kwenye kitabu chake kinachoitwa ìmakabilaî amefafanua sana hili
WAMEFUMANIA AKIZINI
Kauli yao tu inaonekana ni waongo
1. Kundi kubwa la Mafarisayo na Waandishi wakubwa na wadogo walitoshaje kwenye chumba ili kumfumania?
2. Kwa nini hawakumleta mwanamume aliyezini naye?
Nafahamu jinsi uzinzi unavyofanywa na jinsi unavyoweza kutambua
Nikawa nawaza wote waliingiaje kwenye chumba hata wote wakawa kauli moja na hukumu inayofanana?
Wanasisitiza kabisa
ìMwalimu! Mwanamke huyu amefumaniwa alipokuwa katika uzinziî
Wanapotaka kujinufaisha kupitia wewe watakuita kwa cheo
Ndani ya heshima unayopewa kuna ndoana
Ndani ya ufadhili unaopewa kuna mtego
Mwanamume aliyezini naye aliachiwa
Nia ya kumleta mwanamke ni kumtega Yesu Kwa hiyo nia hiyo inaweza kutusaidia kwa nini mwanaume hawakuleta
Inawezekanaje watu wawili wanafanya “dhambi” moja lakini anakamatwa mmoja?
Ndiyo maana nawaogopa sana wanadamu
Ni heri niangukie kwenye mikono ya Mungu kuliko kuangukia mikononi mwa wanadamu
Angalau Mungu ana huruma
Wanadamu wakiamua kukupiga mawe inabidi Yesu ainame ndipo utanusurika
Kinyume na hapo watakupiga mawe mpaka upotee
Wanadamu wakisema hawakupendi ni nadra kuona wamebadili walichoamua
Wakati naangalia jinsi mwanamke alivyokuwa anakaribia kupigwa mawe nikawaza kama kulikuwa na mwingine aliyekuwa kwenye hatari ya kupigwa mawe
Ndio, angalia vizuri.
Kila ukiangalia unaona genge kubwa la watu wamejiandaa kuua bila kuwa na ukweli au ushahidi
Jambo gumu kuhusu kuwa kiongozi ni kuwa na ukweli wa unachosimuliwa
Anayekusimulia ndani yake anajitetea
Ukijikuta katika hali hiyo chaguo sahihi ni kunyamaza
Na mkumbo haukusubiri upate ukweli
Kama unasemwa na unajua anayekusema hana ukweli wenyewe na unajua ukitaka kuvunja ukimya unaweza kueleza ukweli
Tatizo ni kwamba utakuwa peke yako na utakuwa unausema ukweli wakati ambao uongo umeingia kwenye damu wamebeba na mawe
Ni lazima ujizuie vya kutosha kulazimisha ukimya
Na kama ukipoteza uadilifu wako ukafungua mdomo unajua mtavuana nguo
Usichukuliwe na mkumbo
Lile genge lilikosea
Sio tu ukweli wa tuhuma bali walikompeleka
Walimpeleka kwa Yesu
Kama walitaka kumuua wangempiga mawe bila kumpelekea kwa Yesu
Wangemuua kule walikomkuta
Lakini ìwaoî Mafarisayo na Waandishi waliungana wakala njama kumleta kwa Yesu
Wanamleta kwa Yesu? Bora wangemleta kanisani
Watu wengi leo hawajui tofauti ya Yesu na kanisani. Wanadhani wokovu upo kanisani
Matendo 2:47
Wanakuja kanisani lakini hamjui Yesu
Wanakuja kanisani lakini hawana uhusiano na Yesu
Hawasemi haleluya kwa sababu wanaelewa bali ni kwasababu kila mtu anasema Haleluya
Na baadaye wanaimba nyimbo za tenzi kama waliookoka
Walimleta Yule mwanamke mbele za Yesu,
5Katika sheria yetu Musa alituamuru mwanamke kama huyu apigwe mawe. Basi, wewe wasemaje?î
Sasa kama sheria ya Musa iliwaamuru je, kwa nini hawajatekeleza? Kwa nini hawajamuua mpaka sasa?
Wanamtumia Yule mwanamke, aidha apigwe mawe au Yesu na Yule mwanamke wapigwe mawe
Hivi unajua watu wanaweza kukuua unapojaribu kufungua mdomo
Naamini kama walimfumania bila shaka hawakumsubiri avae nguo
Kwa hiyo huyu mwanamke yuko mbele za Yesu akiwa uchi, hajavaa nguo vizuri akijaribu kujisitiri kadri alivyoweza
Anajua muda wowote mawe yanaanza kuelea kichwani
Fikiria kupigwa na mawe na unajua kila aliyebeba jiwe alibeba linalotosha kukuua
Fikiria watu wanakutupia mawe, unachanika ngozi, damu zinamwagika kwenye paji la uso
Wengi wanaokuua hawaanzii tumboni kukupiga bali kihwani wanakupiga mpaka unazimia na hawaachi kukupiga mawe hadi unapotea yanaonekana mawe tu
Uzushi ni ni mawe
Uzushi ni mawe na endapo watu wa kutosha watakurushia baada ya muda hutaonekana
Kinachoweza kuonekana ni ìwamewahi kusikia habari zakoî
Kila unapoungana na uzushi unarusha mawe
Wataandikiana meseji kuhusu wewe na atakayepata atafowadi na mwingine atafowad
Kiongozi usichukuliwe na mkumbo, tafuta ukweli
Walimleta kwa Yesu kwa sababu sheria ilimhukumu kwamba apigwe mawe
Kama Yesu akisema ìhapanaî anakuwa hajaheshimu sheria
Kumbuka kipindi hicho bado sheria ilikuwa haijaondolewa
Hapa Mungu anategwa kwa kutumia Mungu
Aliyetoa sheria za Musa ni Mungu na aliyeletewa mwanamke ni Mungu
Huo ndio wakati wa kuongea kidogo na ukimya uwe mwingi na kwa sehemu kubwa ukimya utoshe kuwa jibu refu na maneno yawe jibu fupi
WOKOVU UNAPATIKANA NJIAPANDA NA MAUTI INAPATIKANA NJIAPANDA
Mungu anaokoa anayemchukia. Mungu akimchukia anayemchukia atakuwa amemchukia anayempenda
Yohana 3:16
Shetani alijua Mungu atamchukia anayemchukia lakini alimwokoa Adamu hata kama alichukia alichofanya
Ndio.
Yesu akisema Musa alikosea, wamemnasa
Akikubaliana na Musa, Yule mwanamke anauawa kwa neno lake
Uongozi ndivyo ulivyo
Maamuzi magumu
Unapokutana fikira mbili zinazokinzana
Kila unalowaza kulifanya lina tatizo mbele yake
Unatakiwa kutafuta njia finyu katikati ili unusurike
Uwapishe bila kumuua Yule mwanamke
Walipomuuliza Yesu wewe wasemaje
Alinyamaza
Kisha akainama na kuandika kwa kidole chini
Anafanya alichofanya Baba wakati wa uumbaji Mwanzoni tunamwona Mungu akifanya kila kitu kwa neno
Wanapodhani wamemnasa Yesu kwa mtego wa zamani na Yesu anatumia njia ya zamani kujinasua
Nguvu ya aya haiko kwenye matamshi bali iko kwenye ukimya na kuinama
Ukimya wa mwalimu ni uwezo wa kutofautina na mkumbo
Inabidi unyamaze wakati kundi kubwa linamshambulia mmoja ili ukimya wako uongee zaidi ya maneno yao
Kwa sababu kama ukimya wake una nguvu basi kuinama kwake kuna nguvu zaidi
Aliinama, aliinamia kisichoweza kuinuka wala kujiinua
Kuinama kwake kunaniambia jinsi Mungu alivyonitoa mbali
Niliposhindwa kufika kwake aliinama
Najua umezungukwa na watu watakatifu lakini Mungu anainama kwa ajili ya mwenye dhambi
Ndivyo ulivyookolewa
Anayekubatiza aliinama
Yesu aliinama Wafil. 2:6
Aliinama kutoka kwenye uungu hadi kuzaliwa kwenye hori
Aliinama kutoka kuwa Mungu hadi kuvaa mwili wa udongo
Kuinama ni Injili, Kuinama ni habari njema kwa mwanamke mwenye dhambi
Kwa mlevi, kwa mwizi,
Aliinama kwa ajili yangu
Ndio maana namwinua
Ni lazima niiname ili aniinue
Unapokuwa kwenye matatizo anainama kwa ajili yako
Ulipojaribu kujinyonga, aliinama kwa ajili yako
Ndio maana inabidi umsifu
Ndio maana inabidi umtukuze
Hukuweza kumfikia, yeye alikufikia
Ndio maana Biblia haisemi Mungu alilipenda kanisa bali “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu”
Unaposhindwa kuomba ipasavyo anainama kukusaidia kuomba
Leo atainama kwa ajili yako
Atakuja ulipo ili aitwe imanuel
Ndio maana Yesu aliandika kwenye mchanga
Bila matamshi alihubiri
Bila matamshi alifanya kwa kuinama
Kwa ukimya alikataa kupeperushwa na mkumbo
Alikataa kuungana na mkumbo ili amfunge mwenye dhambi
Kanisa la leo limepoteza injili
Tunaenda kanisani lakini tumepoteza injili
Leo watu wanahubiriwa mafanikio ya nyumba, kuolewa na magari
Zamani watu walihubiriwa kwa sababu Yesu aliinama ili kuwaokoa
Leo watu hawapigi simu ili ukawahubirie, wanapiga simu kwa sababu wanaumwa ukawaombee
Hawahitaji mahubiri yatakayounganisha kwa Yesu na Kanisa bali wanataka maombi yatakawaunganisha kwenye mali na Kanisa
Tumepatwa na nini?
Anapokuwa jela ndio anahitaji maombi kuliko alivyokuwa anaiba
Usipomwamsha mwanao mapema kwenda kusoma, kwenda kufanya kazi
Ataamshwa kwenda kula, kuoga na kulala akiwa kwenye ulimwengu
Takwimu zinaonyesha 70% ya watoto waliokulia kanisani wana nafasi ndogo ya kuwa wakristo ukubwani kwa sababu kama huoni umuhimu wakiwa wadogo utalazimika kukariri Biblia yote wanakuwa watu wazima
Usiangalie wengine wanaleaje watoto
Usiondoke na mkumbo
YESU HAKUVUNJA SHERIA YA MUSA BILA KUIDHINISHA ADHABU YA KIFO
Mathayo 5:17
Kwenye tukio hili alitakiwa aidha avunje sheria ya Musa au aliruhusu huyu mwanamke kuuawa
Angevunja sheria anpigwa mawe yeye
Hakuvunja sheria na wala hakupigwa mawe na tena mwanamke hakupigwa mawe
Alichofanya aliwaongezea uelewa juu ya nafsi zao
Wakati fulani tunatumia maandiko kuwaua watu kiroho wakati na sisi tuna dhambi zilezile
Tofauti yetu na wale tunaowahukumu ni vile dhambi zetu hazionekani.
ìYeye aisye na dhambi awe wa kwanza kutupa jiweî
Ukimzuia wa kwanza umezuia wa pili
Kwenye mstari huu tunaona kwamba hata kama hawakuwa na dhambi maishani mwao lakini njama iliyotengeneza tukio lile iliwaingiza wote kwenye dhambi
Makosa waliyofanya:
1. Walimhukumu bila uhalali Mathayo 18:16 Waliingia moja kwa moja kwenye adhabu Kumbu. 19:15
2. Walimleta ahukumiwe adhabu kwa Yesu wakati kwa Yesu hakuna hukumu ya adhabu Warumi 8:1
3. Wanamleta ambako hakuna adhabu
Najaribu kuwaza kama kulikuwa na ukweli wa tukio lenyewe la uzinzi
Mwizi huja ili kuharibu na kuua lakini Yesu alikuwa kutafuta na kuokoa kilichopotea
Baada ya kuwaambia asiye na dhambi awe wa kwanza kurusha jiwe hakungoja aone mawe na hakungoja majibu bali aliinama
Huyu ndio kiongozi tunayemfuata
Kwa sababu ukipanda mbegu unatakiwa usubiri mbegu iote usiifukuefukue kuona kama inaweka mizizi
Na Biblia inasema:
Wakashitakiwa na dhamiri zao 1 Yohana 3:20; 1 Tim. 4:2
Wakati anaendelea kuandika chini walihukumiwa sio walijihukumu bali walihukumiwa
Walimhukumu mwenye dhambi walihukumiwa na dhamiri zao
Mungu akusaidie uwe na dhamiri iliyo hai isiwe imekufa ganzi
Ruhusa ya kumpiga mawe iliambana na sharti lililowafanya wafikirie
Kwa hiyo awali walimhukumu bila kufikiria kama ni kweli madai ya tuhuma zao
Walimhukumu kwa mkumbo
Kitu kimoja ambacho rafiki na ndugu zako hawataki ufanye ni kutumia kichwa chako
Hawataki utumie akili zako
Mkumbo
Watu wanaochukuliwa na mkumbo ni wale walioshindwa kufikiria
Walimleta mwanamke ahukumiwe na Yesu lakini kumbe walijileta wahukumiwe wenyewe
Kanisa linataka watu walifuate lakini halitaki watu wafikirie
Viongozi wengi hawataki watu wafikirie
Tofauti iliyopo kati ya werevu na wapumbavu ni msitari mwembamba unaoitwa
Kufikiria
Mkumbo unakuzuia kutafakari
Wanataka uwaige lakini hawataki utafakari
Wanataka uwange mkono lakini hawataki utafakari
Ukihoji wanakufukuza, wanakuwekea watu wakupeleleze
Kanisa halipaswi kuwa mkumbo, hampaswi kuchukuliwa na mkumbo
Mkumbo ni upepo, usichuliwe na upepo
Yesu anawapa watu muda wa kutafakari ili waone kama hawana dhambi
Anawapa nafasi hiyo hata wazee (viongozi) waliowazuia vijana kufikiria
Wanaokuzuia kutafakari sio tu wanazuia usitafakari uhalali wa dhambi wanayomshutumu mtu fulani bali wanajua ukitafakari utagundua wanayemhukumu anaonewa na wao ndio wana dhambi walizoficha
-Njia ya kujilinda ni kushambulia
Ndani ya hukumu kuna dhambi ya hakimu
Alipowaambia aanze wa kwanza kutupa jiwe, Walikumkumbuka dhambi zao wakasahau mawe mkononi
Kutafakari kunakusaidia kukumbuka
Anayekuzuia kutafakari anakuzuia kukumbuka
Anakuzuia usiwe na uhusianoo mzuri na Mungu Zaburi 1:1-4
Ndio maana nawaambia wazee kwamba huwezi kuwa na mvi bila kufanya dhambi
Lakini ajabu Biblia inasema;
Waliomleta mwanamke walikuwa wazee na wadogo
Ningetarajia wazee wasitajwe, Nilitarajia vijana wasifundishwe unafiki na kijisahau
Unapofundisha vijana watu kwamba fulani wana dhambi na kesho wanakuta wewe una dhambi ambayo hawakuwahi kuiona wanakuwa wana wa jehanam mara mbili yako
Hapo ndipo watu wa kanisani wananishangaza jinsi wanamvyosahau haraka mtu wanayemwona kwenye kioo
Haki yako isijengwe juu ya huzuni ya watu wengine
Huruma ileile anayohitaji mwenye dhambi unayemhukumu ndiyo huruma ile anayohitaji mwanao
Ni muhimu kuwaelewa watu kwa sababu usichokielewa kina kawaida ya kujirudia
Usiondoke na upepo
Matajiri wana mkumbo
Maskini wana mkumbo
Unakumbuka wale nguruwe 2000?
Ndio, Usichukuliwe na mkumbo, mkumbo ni kundi ulilotoka nalo mbali
Kundi litakupeleka korongoni usipotafakari
Kufuata upepo kutakufanya ufe kabla hujazeeka
Biblia inasema Kundi la nguruwe likatumbukia majini
Kufuata mkumbo kutamaliza maisha yako kabla hayajaanza
Kufuata mkumbo kutakufanya uumize na kuwachukia watu
Kufuata mkumbo kutakufanya ujitenge na watu ambao kiukweli hawana kosa
Yatakupata haya kwa sababu hutaki kutumia nywele zako
DODONDOSHA MAWE ILI MABADILIKO YAJE
Alipoinuka akakuta mawe tu watu wameondoka
Walipodondosha mawe mabadiliko yalianza ndani yao.
Kumuua mwenye dhambi hakuwezi kukuletea mabadiliko (transformation)
Nakupa changamoto hii leo tuone kama unaweza kudondosha mawe uliyokuja nayo bila kuyarusha
Mabadiliko ya nafsi yako hayaanzi kwa kwenda kwenye makongamano makubwa
Hata ukienda kwenye kongamano ambalo walimu ni malaika kama huwezi kuacha kuhukumu wengine huwezi kubadilika
Kanisa haliwezi kubadilika kwa kuitisha mikutano ya Africa, Ya Tanzania nzima
Ya Africa Mashariki n.k
Vijana hawawezi kubadilika hata kama watakusanywa kwenye makambi, kwenye semina za kitaifa na kikanda kama hawawezi kuwaona wazee wao wanajihukumu na kuacha kurusha mawe
Mawe ni uzushi
Mawe ni hukumu ya uongo
Mawe ni majungu
Mawe ni ufarisayo!
Dondosha mawe!
Kila mtu anaweza kukuchoka kama ambavyo unawachoka wengine,
Lakini usipojichoka mwenyewe huwezi kubadilika
Hadi utakaposema sasa basi Luka 15:17-18
KIla mtu alijisemea
ìkama atapigwa kwa mawe sawa lakini sio jiwe languî Kumpiga mawe ni kujipiga mawe mwenyewe kwa kuwa ni dhambi kama yeye japo dhambi yangu haionekani
Natambua kwamba na mimi ni mwanadamu”
KANUNI YA KIROHO KWA MTU WA ROHONI:
ìNdugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lolote ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole huku ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe. Mchukuliane mizigo na kutimiza sheria ya Kristoî
Yohana 3:16
1Yohana 3:16
Yohana 13:34
Unapomhukumu mtu bila kumrejeza ni uthibitisho tosha kwamba wewe sio mtu wa rohoni
Watu wengine wa namna hii wanatembea na mawe mfukoni, wanangoja wapate mwenye dhambi wayatumia
Wakati fulani unakuwa hujakosea lolote ila kwa vile wanataka kuutumia uzushi kukupaka usoni rangi nyekundu basi watakupaka mpaka hutaonekana kabisa
Wagal. 6 inatufundisha kwamba alighafilika hawi rohoni naye anamhukumu aliyeghafilika hawi mtu wa rohoni Kanisa linakuwa na watu wawili walioghafilika wakati lina mtu mmoja ambaye kanisa limeaminishwa kwamba ana dhambi
Kuna mwingine anakula meza ya Bwana na mwingine inaaminika ametengwa
Kama unajitambua kuwa kiongozi, kama Yesu alivyojitambua utafumba mdomo unaokufanya urushe mawe
Usingoje dhamiri ikufunge mdomo
Watu wenye dhamiri ndio wanaoomba msamaha. Wenye kiburi na kujiona dhamiri zao zilishakufa ganzi. Wanajiona wako mbinguni wakati vichwa viko duniani
Biblia inasema,
Mtu wa rohoni anatakiwa kujiangalia, anatakiwa kujihoji
Anatakiwa kujichunguza
Nilidhani ukiwa mtu wa rohoni huna haja ya kujichunguza, kumbe ukiwa wa rohoni unatakiwa kujichunguza kabla ya kuchunguza
Unatakiwa kujihoji kabla ya kuhoji
Unatakiwa kujiangalia kabla hujaangalia
Fanya hivyo kama kingozi na Mkristo kabla hujawahukumu wengine
Kwa watu rohoni sio kukodolea macho wengine, bali kujiangalia wewe kwanza
Amen!
UMRI HUAMUA MWELEKO MZURI NA MBAYA
ìMmoja mmoja waliondoka kuanzia mkubwa hadi mdogoî
Kuanzia wazee hadi vijana
Tunaonyeshwa hadi umri waliomuhukumu Yule mwanamke
Umri ni uzoefu, umri ni hekima
Walidondosha mawe!
Inamaana waliokuwa mbele na mawe ni vijana, na wazee walikuwa nyuma
Kila anayetumwa anakuwa mbele, anayetumwa hahoji na hatumii akili yake
Vijana walikuwa mbele
Wafadhili walikuwa nyuma
Sijui kama umeokota mawe mwenyewe au umeletewa
Sijui kama umeamua mwenyewe kumchukia mtu au umeshinikizwa lakini nakuona una mawe mkononi
Sijui kwa nini watu wengine huwasalimii wakati hawajakukosea lakini kwa vile wameikosea team yenu
Tunalazimisha rafiki zetu wasiongee na mtu ninawachukia
Iwe kwa akili zako au kwa kuambiwa, unatakiwa kudondosha mawe leo
Wa rohoni hawamhukumu mtu kwa mawe bali kwa upendo
Unajiona una haki kuliko watu wote?
Unajiona unaona una hekima sana? Dondosha mawe bila kurusha
Ukomavu wako haufanani na bei ya mawe uliyoshika, dondosha!
Utumishi wako unalemewa na mawe uliyoshika, dondosha!
Huu sio ujumbe wa kupigiwa vigelegele ni ujumbe wa kujihukumu
Ni ujumbe unatakiwa kukufanya udondoke bila kumrukia mwenye dhambi
Sio kufaidika na upweke wa mtu kwa sababu tu una mawe mkononi
Mawe sio kwa ajili ya watu wa rohoni kuyatumia
Usitumie taarifa ya uongo kuua heshima ya mtu
Usitumie uzushi wa wazushi kuua huduma
Uzushi ni mawe! Dondosha!
Unatarajiwa kuwa na nguvu ya kutosha kuchukua mzigo wa nduguyo.
” Mchukuliane na kuitimiza sheria ya Kristo.”
Tatizo liliko kati ya mwenye dhambi na waandishi na mafarisayo ni dhambi ya mafarisayo na waandishi
Dondosha mawe!
Unajivuna una nguvu kwenye eneo la udhaifu wa ndugu yako wakati alitakiwa ajione mwenye nguvu eneo la nguvu zako
Lakini una mengi wasiyoyajua watu, ndio maana kwako kudondosha mawe ni vigumu kuliko kuyaweza mfukoni
Mawe hayadondoki kirahisi kwa sababu baadhi yetu tumetoka kwenye familia zinazorusha mawe kirahisi kuliko kudondosha
Mawe hayadondoki kirahisi nyakati ambazo ukweli unafichwa kwa faida ya kumuumiza mtu asiyejitetea
Kinachonishangaza kwenye aya hii ni jinsi walivyoondoka
Waliokuwa nyuma walikuwa wa kwanza kuondoka na waliokuwa mbele walikuwa wa mwisho kuondoka tena mmoja mmoja sio kama kundi
Walipoona wazee wanaondoka na vijana waliondoka
Wazee wanapoondoka hawakukanyaga mawe, vijana wanapoondoka walikanyaga mawe ya wazee
Kumbuka mawe ni majungu, uzushi, uongo, hila na fitina
Vijana wanapaswa kuishi ili waone maisha lakini wametangulizwa kurusha mawe
Wazee hawakujua kuwa kuna gharama ya kujihukumu na kuondoa walichoweka kwenye vichwa vya vijana
Yesu alipoinuka alimuuliza Yule mwanamke
ìwako wapi washitaki wako?î 1 Petro 5:8
Hili ni swali ambalo tunaita rhetorical question
Ni swali ambalo anayeuliza anajua jibu
Ni swali analilohitaji mwenye kuulizwa kuliko jibu analohitaji anayeuliza
Mfano:
Ubatizo wa Yohana ulitoka wapi?
Tumtii Mungu au mwanadamu?
Unadhani Yesu hakujua jibu?
Hata kama aliinama, hata kama hakutumia uwezo wake wa Uungu, lakini angalau alisikia mawe yanadondoka
Lengo la swali lilikuwa ni kumfungua Mwanamke
Kwa wale wanaoongelea mambo yaliyopita miaka 10 iliyopita yameacha makovu ambayo ni hali inayokukandamiza hata huwezi kuinuka kumwangalia Yesu
Msongo wa mawazo unakufanya usiamini kama maadui wameondoka
Unakuwa na msongo wa mawazo unaotokana na ulichofanyiwa miaka 30 iliyopita kana kwamba umefanyiwa leo
Habari mbaya ni kwamba unapumua leo lakini unaishi miaka 30 iliyopita
Habari njema ni kwamba yupo Yesu aliyeinama, na washitaki wako wameondoka,
Kwa hiyo swali la Yesu lililenga kumfanya mwanamke atamke kwa kinywa chake ili afunguliwe Warumi 10:8-10
Haijalishi Yesu alimwaga damu kiasi, usipokiri kwa kinywa chako kwamba hakuna wa kukutenga na Yesu, kila siku utahisi una hatia
Warumi 8:39
Alitaka atamke mwenyewe kwamba wameondoka, hawapo
Huko ndiko kufunguliwa
Kufunguliwa ni kujitambua
Huyu mwanamke amedhalilishwa hadharani, Heshima yake imedhalilishwa
Yesu anamfugua kwenye mateso ya udhalili aliofanyiwa
Haiishi mpaka useme imeisha
Mungu amenituma nikwambia kwamba umefunguliwa, uko huru, ya zamani hayakushikilii. Damu yake ilikufungua
Yeye ambaye mwana amweka huru yu huru kwelikweli
Shetani amechanganyikiwa muda huu kwa sababu alitaka uendelee kugalagala chini
HATUA YA MWISHO YA KUMFUNGUA
Kisha Yesu anasema
ìHata mimi sikuhukumuî
ì Nenda usitende dhambi tenaî
Anaondoka na pengine hakupita njia ileile lakini alirudi kule kule walikomtoa
Safari hii atawakuta bila mawe
Atakuta wamehukumiwa na kufungwa na dhamiri wakati yeye yuko huru
Ili Yesu akwambie sikuhukumu ni lazima useme washitaki hawapo
Kuwa Mkristo sio kuwa maarufu, sio kuwa kundi kubwa
Kundi alilokuja nalo limeondoka naye inabidi aondoke peke yake akiwa angalau amesikia mambo matatu ya kumfungua
1. Washitaki wako wapi
2. Sikuhukumu
3. Nenda usitende dhambi tena
Kama unataka kuwa mtu wa rohoni usiondoke na kundi
Kama unataka kuokoka usiende na kundi
Unapoona umebaki peke yako jua mbele yako yupo Yesu
Unapoondoka, Yesu anabaki na mawe waliyadondosha washitaki
Washitaki walipoondoka waliacha mawe,ili yakukumbushe maumivu ya kudhalilishwa, Usibaki yalipo mawe
Mathayo 11:28-20
1 Pet. 5:6-8 Mwanamke na Yesu
Mwanamke anaondoka anaacha mawe yamebaki na Yesu
Yesu akiondoka anayacha mawe peke yake
Usipokuwa mwangalifu utakuwa kama ìwaoî ìnaoî
Lakini Mungu ameniambia nikwambie
USIONDOKE NA MKUMBO
GLOBAL CHURCH OF CHRIST JESUS TANZANIA
IDARA YA UMISHENI NA ELIMU
Limeandaliwa na Willy Emmanuel